Thursday, May 31, 2012

Waliohusika Vurugu Zanzibar Wachukuliwe Hatua

Moja ya kanisa lililochomwa moto katika vurugu hizo likionekana kwa nadani

BAADA ya vurugu na maandamano  na kuchomwa moto baadhi ya makanisa zilizosababishwa na Kikundi cha Uamsho,Serikali imetakiwa kuunda tume ya kukichunguza kikundi hicho chenye mwuelekeo kama Al-Shabab cha nchini Somalia.
Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kiislam (TIPF), Sadiq Godigodi, wakishirikiana na  mwanaharakati Chifu Msopa jijini Dar es Salaam jana kuwa wanalaani vugurugu zote zilizosababishwa na kikundi hicho.
"Watanzania tunapaswa kuwa makini na Kikundi hiki kwani sisi tukiwa Waislam tunaifahamu vizuri historia ya Al-Shabab ilivyoaanza kwani walianza kama hivi sasa hatutaki kuingiza nchi hii katika matatizo ya kuuwana kama ilivyotokea nchini Rwanda 1994"alisema Godigodi. 
Alisema wanaitaka serikali kukichunguza kikundi hicho kwa kuwa kinakwenda kinyume na malengo yake, kwani kilianzishwa kwa ajili ya kufanya mihadhara, kueleimisha, maadili ya dini, kufanya ibada  na mambo yote anayohitaji Mungu (Alla SW).
Aidha, wanalaani vurugu zote zilizosababishwa na baadhi ya watu wa Uamsho kwa kusema makanisa hayakutendewa haki hata kidogo kwa kuwa kanisa si serikali wala Tume ya Uchaguzi au Chama cha siasa.
Godigodi alikwenda mbali kwa kusema wanawalani wale wote wanaopinga muungano kwani hata Mwenyezi Mungu anawachukia wote wanaotaka kujitenga au kufanya ubaguzi wa aina yeyote ya Dini, Kabila au rangi, kwani Mwenyezi Mungu  aliwawakea misingi ya kuheshimu dini za watu wengine na wale wasiokuwa na dini.
Godigod alisema Waislama wanakishangaa kikundi hicho kwa kufanya mihadhara ya kuleta chuki kwa baadhi ya Waislama wa Zanzibar kama vile kupinga muungano wa Zanzibar na Tanganyika wakati kuna utaratibu  umewekwa wa kutoa maoni kuhusu suala hilo.
Vile vile kuwakataa baadhi ya watu kutoka Bara wanaoishi kuondoka  Visiwani humo kama walivyosoma katika vyombo vya habari (huu ni ubaguzi), na kupinga utoaji wa maoni kuhusu mchakato wa Katiba mpya. 
Hata hivyo, alisema Zanzibar ni Kisiwa chenye idadi kubwa ya waislam na vyama vikubwa vyenye idadi kubwa ya wanachama ambapo vyama hivyo vina ushawishi kwa wananchi mbalimbali.
Alisema baada ya muafaka wa CCM na CUF Wazanzibar wamekuwa kitu kimoja wakishirikiana kwa kila jambo ni dhahiri kwamba kila Mzanzibari anhitaji maisha ya umoja na ushirikiano.
Hata hivyo kuna taarifa kuwa Serikali ya Mapinzi Zanzibar imesimamisha shughuli zote za  Kikundi hicho cha Uamsho.

No comments:

Post a Comment