Thursday, May 17, 2012

WAMLILIA MAFISANGO POLENI WANA MSIMBAZI

Mkurugenzi wa mtandao wa Fullshangweblog Bw. John Bukuku kulia akimsikiliza Katibu Mkuu wa timu ya Simba Bw. Evodius Mtawala wakati alipokuwa akielezea mipango ya kuuhifadhi na kuusafirisha mwili wa mchezaji wao marehemu Patrck Mafisango Mutesa aliyeafiki alfajiri ya usiku wa kuamkia leo maeneo ya Chang'ombe Veta jijini Dar es salaam,  wakati akirejea nyumbani kwake na kusababisha watu wengine aliokuwa nao kupata majeraha.

Bw. Mtawala amesema hayo katika hospitali ya taifa ya Muhimbili na kueleza kwamba kwa sasa wanawasiliana na Ubalozi wa Rwanda na mashirika ya ndege ili kukamilisha utaratibu wa vibali mbalimbali tayari kwa kuusafirisha mwili wa marehemu kwenda nchini Rwanda kwa mazishi na taarifa kamili ya lini utasafirishwa itatolewa kesho mara baada ya kukamilika kwa taratibu zote, katika picha kushoto ni Bw. Mwakitalima  mmoja wa mashabiki wa Simba aliyefika muhimbili kushuhudia kilichotokea.

No comments:

Post a Comment