Monday, November 5, 2012

MASSAWE AZINDUA MNARA WA VODACOM KISIWA CHA GOZIBA


Wakazi wa Kisiwa cha Goziba Kilichoko Wilayani Muleba wamekombolewa na kampuni ya mawasIliano ya Vodacom Tanzania baada ya kampuni hiyo kuzindua mnara wake wa mawasiliano katika kisiwa hicho ambapo wananchi sasa wanaweza kuwasiliana popote Tanzania na duniani kwa kutumia mtandao wa mawasiliano wa Vodacom.

Mnara wa Vodacom Kisiwani Goziba ulizinduliwa jana tarehe 30/10/2012 na Mhe. Kanali Mstaafu Fabian I. Massawe aliyembatana na Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhe. Lembrisi Kipuyo. Pia Katika uzinduzi huo Kampuni ya Vodacom iliwakilishwa na Salum Mwalimu ambaye ni Meneja Mahusiano ya nje wa Kampuni hiyo.

Katika Uzinduzi huo Meneja Mahusiano ya nje wa Vodacom Salum Mwalimu aliwaomba wananchi wa kisiwa cha Goziba kuulinda na kuutunza mnara huo kwani alisema kuwa mnara huo umejengwa kwa gharama kubwa, ni zaidi ya mara mbili ya gharama ya kujenga mnara mmoja katika eneo la nchi kavu. Pia aliwahakikishia wananchi wa Goziba kuwa huduma nyingine mbalimbali kama M- Pesa zitapelekwa kwao.

Wananchi wa Kisiwa cha Goziba ambao ni 6000 pamoja na kuchangia asilimia 25 ya pato la wilaya ya Muleba, walisema kuwa kabla ya mnara huo hawakuwa na aina yoyote ya mtandao wa simu, pia bado wanakabiliwa na changamoto katika huduma za kijamii kama shule, Zahanati, na maji safi na slaama. Vilevile usafiri wa kuaminika na kukumbwa na ujambazi wa mara kwa mara na kunyanganywa mali zao.

Wananchi hao waliishukuru Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kuwakumbuka kupitia mbunge wao Charles Mwijage wa Jimbo la Muleba Kasikazini kuwawekea mnara huo ambao utawatatulia baadhi ya kero zao kama kero ya ulinzi kwani itakuwa rahisi kutoa taarifa za uharifu kwa haraka sana pale unapotokea.

Mkuu wa Mkoa alisistiza sana wananchi hao kuutumia mtandao huo kwa manufaa yao na taifa lakini siyo kutumia simu zao kwa mambo ya uhasherati kwani UKWIMWI bado unatisha sehemu za visiwani. Aliwasistiza wananchi hao kuwa waaminifu walioko kwenye ndoa, kutumia kinga na vijana kusubiri muda wao wa kuoa ndiyo waoane. Pia Mhe. Massawe alitumia muda huo kuwagawia kinga (kondomu) wananchi hao na kuwashauri kuzitumia ili kupanga uzazi na kujikinga na virusi vya UKWIMWI.

Vodacom Tanzania tayari pia imetoa Tshs. 4,200,000/= kwa ajili ya ujenzi wa zahanati, pia Mkuu wa Mkoa naye alitoa Tshs 500,000/= ili kuendeleza jengo la zahati ya Goziba ambalo limefikia hatua ya Msingi. Changamoto ni vifaa vyote vya ujenzi kupatika na nje ya kisiwa hicho hata matofari ya kujengea yafyatuliwa Mwanza na kuletwa kisiwani humo isipokuwa mawe tu.

Mnara wa Vodacom siyo tu ni faida ya wakazi wa Goziba na visiwa vya jirani isipokuwa imekuwa mkombozi kwa Manahodha wa mitumbwi iliyokuwa inapotea mara kwa mara na kujikuta sehemu nyingine kwasababu ya kisiwa hicho kutoonekana kwa mbali. Mnara huo umekuwa ndiyo dira ya nahodha wanaokwenda huko kwasasa.

Wilaya ya Muleba inavyo visiwa 36 na 24 tu ndivyo vinakaliwa na wananchi. Pia serikali ianaendelea na juhudi za kuhakikisha huduma za kijamii zinapatikana katika kisiwa hicho ambapo inatarajia katika miaka miwili ijayo itakuwa tayari imeanzisha kituo cha Polisi kisiwani humo.

Imeandikwa na : Sylvester Raphael
Afisa Habari Mkoa
KAGERA @2012

 
MASSAWE AFANYA MAAJABU ATEMBELEA KISIWA CHA GOZIBA

Mandhari ya kisiwa cha Goziba.

Salum Mwalim Meneja Mahusiano ya Nje wa Vodacom Akiongea na Wananchi wa Kisiwa cha Goziba.

Mkuu wa Mkoa kanali mstaafu Fabian Massawe, Katibu wa CCM, Kagera na Salum Mwalim Meneja Mahusiano ya Nje wa Vodacom na RPC Kagera Philipo Karangi Wakiwasili Kisiwani Goziba, Massawe ni mkuu wa mkoa wa kwanza mkoani Kagera kutembelea kisiwa hicho tangu nchi ipate uhuru.

Saturday, November 3, 2012

Mamlaka Ya Mapato Kagera Yazindua Wiki Ya Mlipa Kodi

Baadhi ya maoofisa wa mamlaka ya mapato mkoani Kagera wakisikiliza hotuba ya ufunguzi iliyokuwa inatolewa  na mkuu wa wilaya ya Bukoba Bi Ziporah Pangani.

Mmoja wa maofisa wa TRA

Mkuu wa wilaya ya Bukoba Bi Ziporah Rion Pangani akitoa hotuba ya ufunguzi wa wiki ya mlipa kodi ulifanyika kwenye ukumbi wa chama cha msalaba mwekundu.

Mameneja wa TRA, kulia ni Bw. Mgimba na kushoto ni Magere.

KIKAO CHA MTANDAO UNAOYAUNGANISHA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KAGERA

 Dr George Buberwa akiongea wakati wa kikao cha mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali Kagera KANGONET  kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Kagera.
 Wajumbe halali wa KANGONET.
 Wajumbe wengine.

 Bw. Kiiza alikuwa mmoja wa walioudhuria kikao cha KANGONET, wajumbe wa mtandao huo walikuwa wakulalamikia uongozi ulioko madaraka ambao ni pamoja na Katibu Christan Byamungu na mwenyekiti Yusto Mchuruza, walisema viongozi hao hawana imani nao.
 Kimani na Michael.

Afisa maendeleo ya jamii mkoani Kagera Charles Mwafimbo ndiye aliyeongoza kikao hicho.

JK: Azindua Taasisi Sayansi Na Teknolojia Ya Chuo Kikuu Cha Nelson Mandela Arusha

Rais Jakaya Kikwete, akikata utepe kuweka jiwe la Msingi ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Chuo cha Kikuu cha Nelson Mandera, jijini Arusha, Novemba 02, 2012. Kushoto kwake ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Chuo hicho, Dkt. DMohammed Gharib Bilal. Kushoto ni Makamu wa Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Burton Mwamila
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandera, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu wakati wa hafla ya uzinduzi wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Chuo cha Kikuu cha Nelson Mandera, jijini Arusha , Novemba 02, 2012. Kulia ni Rais Jakaya Kikwete, aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo

 Rais Jakaya Kikwete, akifunua kitambaa ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Chuo cha Kikuu cha Nelson Mandera, jijini Arusha, Novemba 02, 2012. Kulia kwake ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Chuo hicho, Dkt. DMohammed Gharib Bilal. Kulia ni Makamu wa Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Burton Mwamila.
 Rais Jakaya Kikwete, akipokea zawadi ya picha kutoka kwa Makamu wake na Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandera, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Burton Mwamila, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Chuo cha Kikuu cha Nelson Mandera, jijini Arusha
                       
                                     Picha na OMR

Magazeti

Wabunge Vinara Wa Rushwa Hatarini




 BUNGE limeandaa kanuni za maadili ili kuwadhibiti wabunge ambao wanatumia mianya ya kanuni zilizopo kufanya makosa mbalimbali ikiwamo kujihusisha na vitendo vya rushwa. 

Habari zilizopatikana mjini Dodoma na kuthibitishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Shughuli za Bunge, John Joel zinaeleza kuwa hatua hiyo ya Bunge inatokana na kuongezeka kwa wabunge kutuhumiwa kwa makosa mbalimbali wanayoyafanya wakiwa nje na ndani ya Bunge. 

Joel alisema masharti hayo mpaka sasa yapo katika hatua ya kuchapwa na kwamba muda siyo mrefu maadili hayo ya kanuni yatatoka. “Tupo katika hatua ya kuichapa code of conduct (Kanuni za maadili) hiyo na kwamba muda si mrefu itatoka na kuanza kutumika.”

 Alisema wamegundua kuwa baadhi ya wabunge wanatumia kanuni za Bunge zilizopo kuzikwepa na kufanya mambo yasiyofaa ambayo yanashusha hadhi ya Bunge, hivyo masharti hayo mapya yatawabana zaidi.

 Kauli hiyo ya Joel inakuja siku mbili baada ya kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa madai ya kutoa rushwa kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa Jumuiya ya Wazazi uliomalizika jana mjini hapa. Zungu ambaye pia ni Mbunge wa Ilala, alikamatwa na makada wengine wa chama hicho saa 4:30 usiku katika kituo cha mafuta akidaiwa kujaribu kutoa rushwa ya Sh100,000 kwa wajumbe wa mkutano huo wa wazazi. Hata hivyo, Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, Eunice Mmari juzi alikaririwa akisema vijana wake walimtia nguvuni Zungu katika Hoteli ya Golden Crown akiwa na wapambe wake wakiendelea kugawa fedha kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa wazazi.

 Mbunge mwingine ambaye ana kesi mahakamani kwa tuhuma za kujihusisha na rushwa ni Omar Badwel wa Bahi. Badwel anatuhumiwa kuomba rushwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkuranga mkoani Pwani, Zipora Liana.

 Hatima ya Zungu, Badwel Kuhusu kukamatwa kwa Zungu, Mkurugenzi huyo wa Idara ya Shughuli za Bunge, alisema kuwa Bunge halitamchukulia hatua yoyote na badala yake linaviachia vyombo vya dola vifanye kazi yake. 

Joel alisema suala la Zungu bado ni tuhuma hivyo, ataendelea kuwa Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala hadi hapo kama itathibitika kuwa ametenda kosa mahakamani. Alisema suala lake ni sawa na la Mbunge Badwel ambaye ana kesi mahakamani ya kutuhumiwa kujihusisha na rushwa, lakini bado anaendelea kuwa mbunge.

 Hatua hii ya Bunge pia inakuja wakati bado ripoti ya Kamati ya Bunge iliyoundwa kuchunguza tuhuma za wabunge kujihusisha na rushwa wakati wa Bunge la Bajeti mwaka huu, ikisubiriwa kusomwa bungeni. Agosti 2, mwaka huu Spika Makinda aliunda kamati ndogo ya kuchunguza tuhuma za rushwa zilizokuwa zikiwakabili baadhi ya wabunge ambao walidaiwa kwamba walihongwa ili kuikwamisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.

 Kuundwa kwa kamati hiyo, kulitanguliwa na tukio la kuvunjwa kwa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini Julai 28, mwaka huu pia kutokana na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo, kujihusisha na rushwa na wengine kutumia nafasi zao kujinufaisha kwa kufanya biashara na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ambalo lipo chini ya kamati hiyo.

 Mabilioni ya Uswisi Katika hatua nyingine, Serikali imeanza kufanya uchunguzi wa kina ili kujua ukweli na kuwachukulia hatua watu wote walioficha mabilioni ya fedha nchini Uswisi. Waziri Mkuu alisema bungeni jana kuwa, mara baada ya uchunguzi huo kukamilika Serikali itatoa taarifa kuhusu uchunguzi huo. Pinda alikuwa akijibu swali aliloulizwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe wakati wa kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu jana asubuhi. 

“Jambo hili kwa uzito wake, tumeanza kulifanyia uchunguzi ili kujua ukweli wake na hatua stahiki za kuchukua, tukimaliza tutatoa kauli kama ilivyo kawaida yetu, “ alisema. 

Mbowe katika swali lake alitaka kujua Serikali imechukua hatua gani kuhusu taarifa za kuwapo kwa mabilioni ya fedha katika akaunti za benki mbalimbali nchini Uswisi ambazo zimewekwa na baadhi ya vigogo serikalini na viongozi wastaafu.

 Katika Bunge la Bajeti lililopita, Kambi ya Upinzani ililiibua suala hilo wakati wa hotuba yao ya Bajeti wakieleza kuwa kuna jumla ya Sh360 bilioni zilizofichwa na baadhi ya Watanzania katika benki mbalimbali nchini Uswisi. 

Taarifa kutoka Benki Kuu ya Uswisi inaonyesha kuwa baadhi ya fedha hizo zimewekwa katika akaunti za vigogo hao na kampuni za mafuta na gesi zilizopo nchini. Jumanne wiki hii, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika alipokuwa akichangia azimio la kuridhia marekebisho ya pili ya Mkataba wa Ushirikiano kati ya Jumuiya ya Nchi za Ulaya na Nchi za Afrika, Caribbean na Pacific (ACP), alisema Serikali iutumie ushirikiano huo kurejeshwa mabilioni yaliyofichwa nchini Uswisi. 

Naye Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akihutubia mkutano wa hadhara Rombo, mkoani Kilimanjaro Oktoba 26 mwaka huu, alimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru), Dk Edward Hoseah, akidai kuwa bosi huyo ameandika barua Uswisi, akieleza kwamba Tanzania haina masilahi na mabilioni ya fedha yaliyofichwa katika benki za nchini hiyo. Hata hivyo, Dk Hoseah alikanusha akisema kuwa tuhuma hizo hazina ukweli wowote.

                                              Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari

Thursday, November 1, 2012

Bukoba Na Senene Tena

 Baadhi ya wakazi wa mji wa Bukoba wakichangamkia senene.
 Wanafunzi hawakubaki nyuma, huyu ni mmoja wa wanafunzi waliochangamkia senene wajianza kuonekana mkoani Kagera.
 Kitoweo hicho kikiwa sokoni.
 Senene wakirandaranda juu ya magunia.

Wafanyabiashara ya senene wakifanya vitu vyao.

Wednesday, October 31, 2012

Maisha Yanaendelea

Tamko La Masheikh Na Wanazuoni Wa Kiislamu




Reactions::

Magazeti Leo Alhamisi









Reactions::

Abdallah Bulembo Mwenyekiti Mpya Wazazi CCM


Wajumbe wa NEC 
Mhe. Zungu
 Mhe. Adam Malima
Mhe.Jasson Rweikiza.
Reactions::

Kongamano La Afya Ya Uzazi Kwa Vijana

 naibu meya wa manispaa gervas ndaki
mratibu wa maadhimisho meshack mollel
Baadhi ya washiriki
wadau kutoka manispaa mshana mbele na mushi aliyekaa nyuma)
  dr mariam mohamed
Na Denis Mlowe - Iringa
 Maadhimisho ya siku ya afya ya uzazi kwa vijana kwa mwaka 2012 yaliyoandaliwa na wizara ya afya kitengo cha uzazi na mtoto kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la AMREF na wadau wengine yamefanyika mkoani Iringa katika ukumbi wa Highland Hall na kuhudhuriwa na rika za watu mbalimbali wakiwemo waandishi wa habari. Maadhimisho hayo yaliyokuwa na kauli mbiu ya "Andaa taifa bora kwa kuwekeza katika afya ya uzazi wa vijana" mgeni rasmi alikuwa katibu tawala wa mkoa aliyewakilishwa na msaidizi wake pia yalihudhuriwa na naibu meya wa manispaa Gervas Ndaki, mkuregenzi wa manispaa na mwakilishi wa vijana yalikuwa na lengo la kuongeza ufahamu kwa vijana katika suala zima la afya ya uzazi kwa vijana. Mratibu wa maadhimisho hayo kutoka AMREF, Ndugu Meshack Mollel amesema kwamba wizara ya afya kupitia AMREF na wadau mbalimbali wamewezesha maadhimisho hayo kufanyika kwa mara ya kwanza mkoani hapa na ni kitu cha kujivunia kwa mkoa wa iringa kwa kuwa mwaka jana lilifayika jiji dar es salaam na litakuwa faida kubwa sana kwa vijana wa mkoa huu katika kujadili na kuwa na ufahamu mkubwa sana katika suala zima la afya ya uzazi kwa vijana na kutetea na kujenga afya bora kwa vijana wote. Afya ya uzazi kwa vijana yamekuwa na mafanikio makubwa sana kwa vijana tangu yalipoanzwa kufundishwa kwani yamefanikiwa kushirikiana kwa vijana katika kubadilishana uzoefu na utaalamu juu ya afya ya uzazi kwa vijana, aidha yamewezesha vijana kujenga uwezo wa kutetea hoja mbali mbali za kuimarisha afya ya vijana katika uzazi Aidha afya ya uzazi kwa vijana ina changamoto kubwa kama kuwa na majukumu kwa wadau kutotekelezwa ipasavyo na mabadiliko ya mara kwa mara ya uongozi katika asasi mbalimbali ni changamoto nyingine katika afya ya uzazi kwa vijana na kutokuwa na chombo cha kitaifa kinachounganisha wizara zote. Mratibu wa afya ya uzazi na mtoto katika manispaa ya Iringa Dr. Mariam Mohamed  amesema kwamba kuna vituo 42 ndani ya manispaa vinavyotoa huduma ya afya ya uzazi kwa vijana. "Vituo hivyo vinakumbana na changamoto ya upungufu wa watumishi wa afya ya huduma rafiki kwa vijana, ushiriki mdogo wa wazazi katika kupata elimu ya uzazi kwa vijana aidha mfumo wa ukusanyaji wa taarifa na vituo kutokuwa na alama ya utambulisho ndio changamoto" alisema Dr Mariam Mohamed Aliongeza kwa kusema matarajio ya manispaa ni kuongeza watumishi katikam vituo mbali mbali aidha kushirikiana na jamii katika kutoa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana na kusimamia takwimu na kushirikiana na wadau wa mikoa Njombe, Mbeya katika elimu ya afya ya uzazi.
Reactions::