Tuesday, May 29, 2012

Meya Amtishia Mwandishi Wa Habari

Na Mwandishi Wetu
Bukoba

MEYA wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba Anatory Amani ameanza kuwatishia amani waandishi wa habari walioko mkoani Kagera wanaojaribu kueleza ukweli juu ya  miradi ya maendeleo ambayo manispaa hiyo inataka kuitekeleza na kwa kushirikiana na wabia.

Katika hali isiyo ya kawaida meya huyo alimkwida tai mwandishi wa habari wa gazeti la Mtanzania,  Audax Mutiganzi na mfukuza ofisini kwake kwa kumsukuma nje kwa nguvu, alikuwa ameandama na ofisa mkuu mtendaji wa benki ya posta nchini Sabasaba Moshingo aliyekuwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani Kagera.

"Toka, toka, toka ofisini kwangu sikutaki unatuandika vibaya wewe ni mtu mbaya kwetu hatukutaki kabisa na kamwe utawahi kukanyaga ofisini kwangu, toka nje ya ufisi yangu maramoja" alisema hiyo huku akinyanyuka kwenye kiti chake na kumkwida mwandishi tai na kumsukuma nje na kufunga mlango kwa nguvu.

Amani alimfukuza mwandishi huyo kwa madai kuwa anaandika habari mbaya zinazohusiana na manispaa hiyo hasa zinazohusina na miradi ya iliyoghubikwa na utata hasa kwa upande wa kanuni na sheria za manunuzi ambayo ni pamojan na ya ujenzi wa soko kuu na wa upimaji wa viwanja.

Meya huyo kabla ya kumfukuza mwandishi huyo alitoa maelekezo kwa kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Bukoba, Steven Nimziirwa alimweleze meneja wa Benki ya posta Maduhu Makoye amueleze mwandishi huyo asiingie kwenye ofisi ya Meya huyo kwa madai hataki kukutana naye.

Nimziirwa alifanya kama alivyoagizwa na meya wake, mwandishi huyo pamoja na taarifa hiyo alikaa kimya akaendelea kutekeleza wajibu wake wa kukusanya taarifa za matukio ya ziara ya ofisa mkuu mtendaji wa benki ya posta nchini.

Mwandishi baada ya kufanyiwa unyama huo na meya alienda moja kwa moja  hadi kituo cha polisi kutoa taarifa juu ya  tukio hilo yenye kumbukumbu namba BU/RB/3161/2012, taarifa hiyo ilifunguliwa kituo kikuu cha polisi.

Meya huyo amekuwa na tabia ya kuwatishia waandishi wa habari, hivi karibuni aliwatishia waandishi wa habari wa kituo cha radio Kasibante kilichoko mkoani Kagera kwa madai ya kuhoji miradi inayotekelezwa na manispaa kwa kushirikiana na wabia.

Amani alipotafutwa ili athibitishe malalamiko yaliyotolewa na mwandishi wa habari simu yake ilikuwa inaita bila kupokelewa, alitumiwa ujumbe mbalimbali wa maandishi kwenye simu yake na waandishi wa habari lakini alikataa kuujubu.

Hivi karibuni gazeti ka Mtanzania lilikuwa likifuatilia kwa karibu miradi ya maendeleo ambayo manispaa inataka kuitekeleza kwa kushirikiana na wabia, gazeti hili lilikuwa linaelezea ukikwaji wa taratibu za manunuzi za kuiteua kampuni ya OGM mwandisi mshauri wa mradi wa ujenzi wa soko kuu la Bukoba.

Katika mradi huo kampuni ya OGM ambayo inadaiwa kutokuwa na sifa za kuufanyia mradi huo usanifu itachota zaidi ya milioni 590.

Mwisho

No comments:

Post a Comment