Tuesday, May 8, 2012

Waandishi Wa habari Kagera Wafundwa na Mkuu Wa mkoa


 
Bukoba
 
Kanal mstaafu Fabiani Massawe ni mkuu wa mkoa wa kagera  amewashauri wanachama na waandishi wote mkoani humu kuandika habari za uchunguzi wakifuata misingi,maadili na kanuni za uandishi wa habari ili kufanya kazi yao kuwa nyepesi na isiyokuwa na migongano isiyokuwa ya lazima.
 
Massawe aliwashauri waandishi kuandika habari za uhakika kwa kutumia vyanzo sahihi kabla ya kuandika habari na kutoandika habari zinazopendelea upande mmoja na zenye maslahi binafsi ili kuepuka kusababisha migawanyiko ndani ya jamii inayoweza kusababisha uvunjifu wa amani   ambapo alitoa mfano wa vita vya Kimbali vilivyosababishwa na uchochezi wa baadhi ya vyombo vya habari huko nchini Rwanda.
 
Aliwataka waandishi kuacha tabia ya kuomba mishiko au bahasha ndipo waandike habari kwa madai kuwa tabia hiyo ni kujidhalilisha na kuonekana waandishi ni watu wa kulalamika kila wakati kuwa hawana kitu jambo ambalo ameziomba klabu na waajiri wa vyombo mbalimbali kulifanyia kazi kwani ni kero inayowafanya watoa habari kujenga uadui na waandishi kwa madai kuwa wamekuwa wakitishia kuwa wakinyimwa mishiko hawaandiki habari ya aina yoyote.
 
Pia amewashauri waajiri wa vyombo mbalimbali vya habari hususani radio za kijamii zipatazo tano za mkoa wa Kagera kutafuta utaratibu wa kuwaondoa waandishi makanjanja ambao wamekuwa wakiajiriwa kwani wanalipwa ujira mdogo huku waandishi wenye ujuzi na kazi hizo wakikosa nafasi jambo ambalo amedai kuwa matokeo yake wamekuwa wakitumia radio hizo kujadili maisha ya watu na kuongea mambao yasiyofaa katika jamii huku wengine wakitangaza habari za mapenzi tu wakati kuna habari zinazogusa jamii mfano wahamiaji haramu na rushwa hazipati nafasi jambo ambalo amedai kuwa ni kuidhalilisha taaluma hiyo muhimu.
 
Kanal Massawe alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za kuadhimisha sikuukuu hiyo ya uhuru wa vyombo vya habari ambapo kwa mkoa wa Kagera ilifanyika katika ukumbi wa Coffee Tree in ndani ya Manispaa ya Bukoba na kudhaminiwa na muungano  wa vilabu vya waandishin wa habari nchi (UTPC)na kuudhuliwa na viongozi mbalimbali wa mkoa huo ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti wa bodi ya kahawa nchini Pius Ngeze,Kamanda wa Takukuru mkoa Domina Mkama,Kaimu kamanda wa polisi mkoa Vitus Mlorele,mkuu wa Wilaya ya Bukoba Samweli Kamote na viongozi wa vyama vya siasa mkoa na Wilaya.
 
Aidha  mkuu huyo wa mkoa aliiahidi kuwachangia kiasi cha shilingi milioni moja kama mchango wa kununulia kiwanja cha kujenga ofisi ya klabu hiyo ili waweze kuondokana na  usumbufu wanaoupata wa kupanga kwenye majumba ya watu ambapoa wamekuwa wakiwasumbua mara kwa mara pasipokuwa na sababu za msing .
 
Katika hatua nyingine klabu ya Waandishi wa habari mkoani Kagera (KPC) imetoa msaada mbalimbali katika wodi za wagonjwa katika hospitalia ya mkoa wa Kagera.
 
Tukio hilo lililifanyika May 5 katika hospitali hiyo kwa kukabidhi misaada mbalimbali katika wodi za watoto hospitalini hapo.
 
Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoani Kagera John Rwekanika alisema kuwa wanachama wa KPC wapatao 34 wamelazimika kutoa misaada hiyo katika tamasha lao lakuadhimisha uhuru wa vyombo vya habari duniani iliyoadhimishwa mei 5 badala ya mei 3 mwaka huu inayoadhimishwa kila mwaka kutokana na wanachama na wanachama wengi kukabiliwa na majukumu mwengi katika tarehe rasmi inayoadhimishwa ulimwenguni.
 
Alisema kuwa misaada iliyotolewa ni pamoja na sabuni,sukari na biskuiti vyote vyenye thamani ya shilingi laki 2 ambapo vyote viligawiwa katika wodi za watoto ambazo alizitaja kuwa ni namba saba yenye wodi mbi A na B tofauti na kuwa jumla ya watoto 55 waliolazwa katika hospitalia hiyo wamepokea misaada.
 
Alisema kuwa waandishi wa habari ni sawa na taasisi au jumuiya yoyote ya kirai inyopaswa kushirikiana na raia katika shughuli zote za kijamii kuwa kutokana na chama chao kuwa na ushirikiano wa dhati wameonelea kutumia fursa hiyo kuungana na wagonjwa,wazazi na wauguzi wa hospitali hiyo.
 
Kwa upande wake kaimu mganga mfawidhi wa hospitalia hiyo Dk.Leonce Mboyerwa alisema kuwa kitendo kilichofanya na waandishi wahabari hao wa Klabu hiyo ni cha kizalendo na kuwa kimeonyesha ni kiasi gani waandishi walivyo na mchango mkubwa katika jamii.
 
Mboyerwa aliongeza kuwa waandishi wa habari wanafanya kazi katika mazingira magumu lakini wameweza kuonyesha moyo wao wa upendo katika maadhimisho yao ya uhuru wa vyombo vya habari kwa kuungana na jamii inayowategemea kuwa hata taasisi nyingine za Kiserikali na zisizo za Kiserikali wanapswa kuiga mfano uliotolewa na wanachama na uongozi wa KPC.
 
Aidha mmoja wa wazazi katika Wodi ya watoto namba saba A Joyce Rweyemamu alisema waandishi wa habari wameonyesha kitendo cha utu na kuwa wameionyesha jamii kuwa wao ni kioo cha jamii.
 
Alisema kuwa pamoja na misaada walioipokea kutoka kwaandishi hao kuwa wawapo katika hospitali hiyo wanakabiliwa na changamoto ya kukosekana kwa madawa na kuwa mgonjwa aliyelazwa analazimika kujinunulia madawa ambapo wagonjwa wengine wanakuwa hawa uwezo wa kujinunulia madawa kuwa jambo hilo linadhiri afya na kusababisha vifo vya mara kwa wagonjwa.
 
Naye mku wa idara ya watoto hospitalia ya mkoa wa Kagera Gerad Kabyemera alikiri kuwepo kwa hari hiyo ya upungufu wa madawa na kuwa tatizo hilo halisababishwi na uongozi wa hospitali balia linasababishwa na stoo kuu ya madawa makao mkauu ya afya Dar Es Salaam.
 
Kabyemera alisema kuwa uongozi wa hospitali unaomba wastani wa asilimia 100 ya madawa kutoka makao makuu lakini wanatumiwa wastani wa asilimia 40 ya madawa walioomba ambayo hayawezi kutosheleza mahitaji ya wagonjwa kulingana na idadi ya wagonjwa wanaolazwa katika hospitali hiyo.
 
 mwisho

No comments:

Post a Comment