Wednesday, October 31, 2012

Maisha Yanaendelea

Tamko La Masheikh Na Wanazuoni Wa Kiislamu




Reactions::

Magazeti Leo Alhamisi









Reactions::

Abdallah Bulembo Mwenyekiti Mpya Wazazi CCM


Wajumbe wa NEC 
Mhe. Zungu
 Mhe. Adam Malima
Mhe.Jasson Rweikiza.
Reactions::

Kongamano La Afya Ya Uzazi Kwa Vijana

 naibu meya wa manispaa gervas ndaki
mratibu wa maadhimisho meshack mollel
Baadhi ya washiriki
wadau kutoka manispaa mshana mbele na mushi aliyekaa nyuma)
  dr mariam mohamed
Na Denis Mlowe - Iringa
 Maadhimisho ya siku ya afya ya uzazi kwa vijana kwa mwaka 2012 yaliyoandaliwa na wizara ya afya kitengo cha uzazi na mtoto kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la AMREF na wadau wengine yamefanyika mkoani Iringa katika ukumbi wa Highland Hall na kuhudhuriwa na rika za watu mbalimbali wakiwemo waandishi wa habari. Maadhimisho hayo yaliyokuwa na kauli mbiu ya "Andaa taifa bora kwa kuwekeza katika afya ya uzazi wa vijana" mgeni rasmi alikuwa katibu tawala wa mkoa aliyewakilishwa na msaidizi wake pia yalihudhuriwa na naibu meya wa manispaa Gervas Ndaki, mkuregenzi wa manispaa na mwakilishi wa vijana yalikuwa na lengo la kuongeza ufahamu kwa vijana katika suala zima la afya ya uzazi kwa vijana. Mratibu wa maadhimisho hayo kutoka AMREF, Ndugu Meshack Mollel amesema kwamba wizara ya afya kupitia AMREF na wadau mbalimbali wamewezesha maadhimisho hayo kufanyika kwa mara ya kwanza mkoani hapa na ni kitu cha kujivunia kwa mkoa wa iringa kwa kuwa mwaka jana lilifayika jiji dar es salaam na litakuwa faida kubwa sana kwa vijana wa mkoa huu katika kujadili na kuwa na ufahamu mkubwa sana katika suala zima la afya ya uzazi kwa vijana na kutetea na kujenga afya bora kwa vijana wote. Afya ya uzazi kwa vijana yamekuwa na mafanikio makubwa sana kwa vijana tangu yalipoanzwa kufundishwa kwani yamefanikiwa kushirikiana kwa vijana katika kubadilishana uzoefu na utaalamu juu ya afya ya uzazi kwa vijana, aidha yamewezesha vijana kujenga uwezo wa kutetea hoja mbali mbali za kuimarisha afya ya vijana katika uzazi Aidha afya ya uzazi kwa vijana ina changamoto kubwa kama kuwa na majukumu kwa wadau kutotekelezwa ipasavyo na mabadiliko ya mara kwa mara ya uongozi katika asasi mbalimbali ni changamoto nyingine katika afya ya uzazi kwa vijana na kutokuwa na chombo cha kitaifa kinachounganisha wizara zote. Mratibu wa afya ya uzazi na mtoto katika manispaa ya Iringa Dr. Mariam Mohamed  amesema kwamba kuna vituo 42 ndani ya manispaa vinavyotoa huduma ya afya ya uzazi kwa vijana. "Vituo hivyo vinakumbana na changamoto ya upungufu wa watumishi wa afya ya huduma rafiki kwa vijana, ushiriki mdogo wa wazazi katika kupata elimu ya uzazi kwa vijana aidha mfumo wa ukusanyaji wa taarifa na vituo kutokuwa na alama ya utambulisho ndio changamoto" alisema Dr Mariam Mohamed Aliongeza kwa kusema matarajio ya manispaa ni kuongeza watumishi katikam vituo mbali mbali aidha kushirikiana na jamii katika kutoa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana na kusimamia takwimu na kushirikiana na wadau wa mikoa Njombe, Mbeya katika elimu ya afya ya uzazi.
Reactions::

Saturday, October 27, 2012

UCHAFUNZI WA MAZINGIRA ZIWA VICTORIA UNATISHA



Wanyama aina ya Punda wakiwa wamebeba mchanga uliokuwa unachimbwa katika ufukwe wa ziwa victoria kwenye mwalo wa Igombe jijini mwanza shughuli nyingi za kibinadamu zinazofanyika katika mwalo huo zinachangia uharibifu wa mazingira


wanahabari kutoka mikoa mbalimbali ya tanzania bara na visiwani wakishuhudia uharibifu wa mazingira baada ya mafunzo ya siku nne mkoani Mwanza

Mwezeshaji wa mafunzo hayo ya uandishi wa habari za mazingira Bw. Deo Mfugale akiwaongoza wanahabari wakati wa ziara ya mafunzo mwalo wa Ibombe ikiwa ni hatua ya mwisho ya mafunzo hayo.

MNYAUKO BACTERIA WATISHIA USALAMA WA NDIZI KAGERA

UGONJWA unaoshambulia migomba wa mnyauko bacteria umeanza kuathiri upatikanaji wa ndizi kwenye maeneo mbalimbali yaliyoko mkoani Kagera.

Ugonjwa huo unasambaa kwa kasi hasa kwenye maeneo ya wilaya za Muleba na Karagwe ambayo uzalisha  ndizi nyingi mkoani Kagera na maeneo mengine ya wilaya za Bukoba na Misenyi.

Hali ya ugonjwa huo unaoshambulia migomba wa mnyauko bacteria imechangbia kupunguza uzalishaji wa ndizi mkoani Kagera jambo ambalo limechangia kupanda kwa bei ya ndizi zinapopelekwa kwenye masoko.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kwamba kwenye soko kuu la Bukoba ndizi kubwa inauzwa kwa wastani wa kati shilingi 15,000 hadi 20,000 ambapo miaka iliyopita ndizi kubwa zilikuwa zinauzwa kwa wastani wa kati ya shilingi 6,000 hadi 8,000.

Kupanda kwa bei ya ndizi iliyochangiwa na ugonjwa wa mnyauko bacteria wa migomba kumewalazimisha baadhi ya wakazi wa mkoa wa Kagera ambao hutegemea ndizi kama chakula chao kikuu kubadilika ambapo sasa wanalazimika kula ugali na wali.

Baadhi ya wakazi wa mkoa wa Kagera wamelazimika kubadili fikira zao za kudhani kuwa ndizi ndicho chakula kikuu baada ya kushindwa kumudu gharama za kununua ndizi kwenye masoko ambazo bei yake ni kubwa.

Baadhi ya wakulima bora wa migomba mkoani Kagera ambao mashamba yao yameathirika kutokana na ugonjwa wa mnyauko bacteria wa mogomba ni pamoja kamishina mstaafu wa jeshi la polisi Alfred Tibaigana.

Kamishina Tibaigana shamba lake liko katika kijiji cha Buganguzi wilayani Muleba limeathirika sana, Mkulima huyu kabla ya ugonjwa huu alikuwa na uwezo wa kuzalisha wastani tani 40 za ndizi kwa wiki ambapo sasa anazalisha wastani wa tani zisizozidi 10 kwa wiki.

Aidha, baadhi ya wakulima mkoani Kagera wameitahadharisha serikali kuchukua hatua za haraka za kuthibiti ugonjwa huu unaosambaa kwa kasi ili zao la ndizi mkoani Kagera lisibaki kwenye vitabu vya historia.

JK Katika Kikao Cha Kazi



 Wajumbe wakichangia katika kikao cha kazi (retreat) cha siku tatu cha Mawaziri, Naibu Mawaziri na maofisa waandamizi wa serikali wanaokutana kujadili mikakati endelevu na utekelezaji wa sasa na wa baadaye katika Ukumbi wa St Gaspar mjini Dodoma
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha kazi (retreat) cha siku tatu cha Mawaziri, Naibu Mawaziri na maofisa waandamizi wa serikali wanaokutana kujadili mikakati endelevu na utekelezaji wa sasa na wa baadaye katika ukumbi wa St Gaspar mjini Dodoma. Pamoja naye meza kuu ni Makamu wa Rais Dk. Mohamed Ghalib Bilali (kulia) na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.



 Rais Jakaya Mrisho kikwete na Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda wakipitia Waraka wa Utumishi Namba 5 wa mwaka 2009 kuhusu matumizi bora na salama ya vifaa na mifumo ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEKNOHAMA) serikalini wakati wa kikao cha kazi (retreat) cha siku tatu cha Mawaziri, Naibu Mawaziri na maofisa waandamizi wa serikali  kujadili mikakati endelevu na utekelezaji wa sasa na wa baadaye katika ukumbi wa St Gaspar mjini Dodoma.



PICHA NA IKULU

Magazeti Magazeti



















Monday, October 22, 2012


RAIS KIKWETE AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA KENYA LEO IKULU DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa  Jakaya Mrisho Kikwete ametaka wananchi wa Kenya wapewe nafasi ya kuamua ni viongozi gani wanawataka katika Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika Machi mwakani.
Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa wananchi wa Kenya wanayo haki ya msingi kabisa kuamua hatma ya taifa lao katika Uchaguzi Mkuu huo.
Mheshimiwa Rais aliyasema hayo leo Oktoba 21, 2012 alipokutana na kufanya mazungumzo na ujumbe wa wabunge wa vyama mbalimbali vya siasa vya nchini Kenya uliomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam.
Ujumbe huo uliongozwa na Naibu Waziri Mkuu wa Kenya na Waziri wa Fedha Mhe. Uhuru Kenyatta ambaye pia ni Mwenyekiti wa  chama cha TNA na Waziri wa Sheria wa Kenya Mhe Eugene Wamalwa wa chama cha New Ford Kenya. Wote wawili ni wagombea wa nafasi ya Urais katika uchaguzi ujao.
Wengine katika msafara huo walikuwa ni Naibu Waziri wa Afya na mbunge wa Mombasa Mhe. Kambi Kazungu, Mbunge wa kuteuliwa wa chama cha TNA  Bi Rachel Shebesh, na Mbunge wa Kajiado kwa tiketi ya TNA Moses ole Sakuda na mbunge wa zamani Mhe Abdullahi Alli.
Rais Kikwete aliwapongeza kwa kuamua kufanya kazi kwa pamoja licha ya kuwa watakuwa  washindani katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu huo.
Mheshimiwa Rais ameitakia heri nchi ya Kenya katika uchaguzi huo ujao, na kusisitiza kwamba nchi hiyo ya jirani ina umuhimu katika mustakabali wa kiuchumi kwa nchi  za Afrika Mashariki.
Rais Kikwete wakati huo akiwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) alikuwa miongoni mwa viongozi walioshughulika sana kutafuta ufumbuzi wa ghasia na vurugu zilizozuka kufuatia Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2007 nchini Kenya.
Rais Kikwete alikaa siku tatu nchini Kenya akitafuta usuluhishi wa vurugu hiyo ya kisiasa nchini humo, ambayo katika mazungumzo yake leo ameyataja kama ajali iliyolipata Taifa la Kenya, na ambayo majirani wake hawaitarajii kutokea katika uchaguzi ujao.
Imetolewa na:
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS
DAR ES SALAAM,