Tuesday, March 27, 2012

UMEIPATA HIYO YA TAKUKURU KAGERA

Na Mwandishi Wetu
Karagwe

OFISA mkuu  wa taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa (TAKUKURU) wilayani Karagwe mkoani Kagera anatuhumiwa  kwa kujihusisha na kudhohofisha  kesi ambayo inawakabili watu ambao ni raia wa nchi jirani ya Rwanda ambao wanabiliwa na kesi ya  wizi wa ngombe  36 walioibiwa mwezi september 2 mwaka 2010 kata Ihembe  wilayani Karagwe.

Akizungumza na waandishi wa habari wilayani Karagwe Gozibath Blandes ambaye ni mfugaji wa kata ya Ihembe na ndie aliyeibiwa ngombe hao alisema kuwa ofisa huyo ambaye anaitwa Onesphor Ajinasi anajihusisha na kesi ambayo haimuhusu kwa kuwatishia wapelelezi wa kesi hiyo wakiwemo mashahidi kwa upande wa mashtaka.

Blandes ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Karagwe (CCM) alisema kuwa hadi hivi sasa kesi hiyo inayoendelea katika mahakama ya wilaya ya Kayanga inaedelea kusikilizwa na mashahidi wanne kwa upande wa mashtaka wametoa ushahidi wao, lakini alisikitishwa na vitendo vya ofisa wa Takukuru kutaka kuingilia uhuru wa mahakama.

Aliongeza kuwa watuhumiwa ambao wanahisika na wizi wa ngombe zake sio Watanzania ni wanyarwanda na aliwataja kwa majina ya Rusagara Geofrey(33) mfanyakazi katika mamlaka ya mapato nchini Rwanda,Joramu Sebatwale(47) na Ndamaji Anacleth (66) ambao wote wanahusika na vitendo vya wizi.

Aidha aliongeza kuwa ngombe hao walikamatwa mnamo tarehe 5/4/2011 katika eneo la Kasulo wilayani Ngara eneo ambalo walikuwa wamefichwa mara baada ya kuibiwa na raia hao wa Rwanda.

"Kwakweli bado inasikitisha kuona mtumishi wa serikali tena kitengo muhimu anaigilia sehemu ambayo hausiki nayo ili kuharibu kesi ambayo ahusiki nayo tena kibaya zaidi anaweka kesi za kubumba kwa wale wote wanasaidia wakiwemo wapelelezi kutoka jeshi la Polisi ambao siwezi kuwataja inabidi mamlaka husika kumuangalia huyo mtumishi wao"alisema Blandesi.

Aliongeza kuwa wananchi wa wilaya hiyo wanakabiliwa na tatizo la wizi wa ngombe kutoka kwa wavamizi wa nchi jirani jambo ambalo linawaathiri wafugaji wadogowadogo.

Aidha taarifa ambazo ziliwafikia waadishi wa habari zinasema kuwa ofisa huyo wa Takukuru wilaya amekuwa akiwaambia baadhi ya wananchi kuwa atahakikisha anawafuatilia wale wote wanajihusisha na kesi hiyo na ikiwezekana anawawekea mitego ya rushwa ya kutegeshea.

Jitihada za kumtafuta ofisa huyo zilishindikana kwa kuambiwa kuwa akuwepo katika eneo la kazi na kwamba yuko mbali na wilaya hiyo nakuambiwa kuwa suala hilo anaweza kulizungumzia kamanda wa Takukuru mkoa.

Akizungumzia suala hilo Kamanda wa Takukuru Mkoani Kagera Domina Mkama alisema kuwa taarifa ambazo zinatolewa juu ya mtumishi wake azina ukweli ndani yake bali ni kikundi kidogo cha watu ambao wanachunguzwa au waliwahi kuchunguzwa na taasisi hiyo na wanataka kuijengea chuki Takukuru.

Alisema suala la kesi ya wizi wa Ngombe analifahamu kwani iko mahakamani kwa hiyo kesi kama sio ya Takukuru ni vigumu ofisa yoyote kuingilia kwaiyo huyu ofisa wake hana mamlaka ya kuingilia kesi isiyo muhusu,hizo ni chuki za baadhi ya watu na jambo hili halipo.

Mwisho

No comments:

Post a Comment