Saturday, March 10, 2012

Tanzania inapongezwa

TIMU ya wataalam wa mpango wa tathimini ya utendaji kazi kwa nchi za Afrika (APRM) imeisifia Tanzania kwamba ni hazina kubwa katika suala zima la utawala bora katika nchi za Afrika na duniani kote.

Profesa Aderic Nade kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni mmoja wa wajumbe wa timu hiyo kati ya 21 wanaounda timu hiyo alibainisha  hayo jana katika  mkutano wa siku moja uliofanyika mjini Bukoba kati ya wadau wa utawala bora na tume hiyo ya APRM kutoka makao makuu.

Prof. Nade ambaye pia ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Lagos kilicho nchini Nigeria,alisema kuwa pamoja na changamoto mbalimbali zinazoikabili Tanzania lakini imekuwa ni kisiwa cha nchi nyingine kuja kujifunzia jinsi gani wanavyoilinda amani yake ikiwa ni sambamba na misingi ya utawala bora inayodumishwa kwa wananchi wake.

Alisema lengo la mkutano huo na dhamila kubwa ya tume ni kuangalia mchakato mzima wa utawala bora katika nchi hii,historia   na masuala mazima yanayopelekea utawala bora ulioko Tanzania ulivyoimalika leo na hata kabla ya uhuru.

Alieleza kwamba umuhimu wa kuwepo APRM ni kuhakikisha Afrika inarudi katika mustakabali wa utawara bora ambapo hari hiyo itajenga misingi mipya ambayo itaegemea katika kujadiri mkataba wa kijamii kati ya Serikali na wadau,Serikali na Raia pia kuweka misingi mipya ya mahusiano kati ya Watu wa Afrika.

Alisema kuhusu suala la demokrasia  katika nchi za Kiafrika ni jambo muhimu ambalo ni ndoto ya nchi za kiafrika wanayohitaji kuipata kwahiyo ni haki ya Raia kuuliza Serikali ni mambo gani inapswa kufanya na kama imefanya imefikia malengo yapi.

Alisema malengo mengine ni kuhakikisha pale jambo linapotokea katika nchi moja wapo katika Afrika lionekane kuwagusa Waafrika wote ambapo aliongeza kwamba hari hiyo haikuanza leo bali ilianzishwa na waasisi wa Afrika ambao ni baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambalage Nyerere,Kwame Nkuruma na Keneth Kaunda.

Alisema kuwa tathimini hii ni endelevu ambapo kila baada ya miezi sita wadau watatakiwa kukaa na kutathimini ambapo kila nchi itatakiwa kutoa taarifa jinsi gani imetekeleza mawazo ambayo yaliibuliwa na wadau na kila baada ya miaka mine timu itafanya tathimini juu ya utawala bora pamoja na uendelevu katika nchi za Afrika.

Kwa upande wa mgeni rasmi katika mkutano huo ambaye pia ni katibu tawala wa mkoa wa Kagera Nassor Mnambila kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo kanal mstaafua Fabiania Massawe alisema kuwa pamoja na mafanikio hayo ya Tanzania kuwa hazina katika utawala bora bali zipo changamoto zinazowakabili kama Serikali.

Mnambila alisema kuwa changamoto hizo ni mauaji ya vikongwe na walemavu wa ngozi (albino) kwa sababu ya imani za kishirikina,ukeketaji kwa watoto wa kike,ujambazi,ukatili wa kijinsia kwa wanawake na ukatili kwa watoto hawajapata uwakilishi wa kutosha katika masuala ya kisheria ambapo amesema kuwa hayo ni baadhi ya changamoto ambazo Serikali inaendelea kupambana nazo.

mwisho

No comments:

Post a Comment