Thursday, March 8, 2012

JANA  KIMEIBUKA KIPINDI KIPYA CHA TV CHA ‘ONGEA NA JANET’

*AITAKA JAMII KUACHA WOGA NA KUJITOKEZA KUONYESHA VIPAJI.

MO BLOG: Nini Theme ya kipindi cha ‘ONGEA NA JANET’..?

JANET: Aah…!! Theme ya “ONGEA NA JANET’ ni kipindi ambacho kinatoa fursa kwa mtu yeyote kuja kuongea ili mradi awe na kitu ambacho kinaweza kuilemisha jamii. Kipindi hiki kinazungumza na watu wa rika zote. Na katika kipindi hiki kwa kweli mimi nazungumzia kila kitu sijajiwekea limitations. Lengo ili tufike mahali tuweze kuzungumza hata yale mambo ambayo watu wanaogopa kuyazungumza hadharani.

Japo watu wengi wanapenda nizungumzie mambo ambayo yapo current, lakini kwa mfano yakitokea mafuriko, ukifungua TV zote taarifa za habari zinazungumzia mafuriko, radio zote ni mafuriko, ukisoma kila gazeti ni mafuriko na hata misemo mitaani inakuwa kuhusu mafuriko. Sikuona tena umuhimu wa kuongelea kitu ambacho kinaongelewa kila mahali, nataka kutoa nafasi ya kuzungumzia mambo ambayo hatupati nafasi ya kuyazungumzia.

Kwa mfano huwezi kukuta, gazeti au TV ikizungumzia kuwa wanawake walioko katika ndoa wanapata taabu kwa sababu ya nyumba ndogo, na hata kama itaandikwa basi inapewa nafasi ndoogo.

Na sifikirii kipindi changu kiishe leo au kesho  hiki kitaendelea siku zote.

MO BLOG: Watazamaji watarajie nini kutoka kwako katika siku zijazo..?

JANET: Watarajie mambo mengi mazuri na kuwa kila siku kipindi kitakuwa na kitu kipya. Nitakuwa na season 4, hivyo kila season itakuwa tofauti na nyingine. Mfumo nitakaotumia katika season 1 utakuwa tofauti na nitakaoutumia katika season 2 na kuendelea.

No comments:

Post a Comment