Friday, April 20, 2012

Viongozi Wa Dini Wafanya Semina Ya Sensa

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Ramadhani Khijjah akizungumza na viongozi  mbalimbali wa dini kuelezea umuhimu na ushiriki wao katika kufanikisha sensa ya watu na makazi itakayofanyika kitaifa mwezi Agosti mwaka huu  wakati wa mkutano wa viongozi wa dini unaoendelea  jijini Dar es salaam.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Ramadhani Khijjah (kushoto) akiandika maswali yaliyoulizwa na viongozi wa dini kuhusu namna serikali ilivyojipanga kukamilisha sensa ya watu na makazi  itakayofanyika mwezi Agosti 2012. Wengine ni mkurugenzi mkuu wa ofisi ya taifa ya takwimu Dkt. Albina Chuwa (katikati) na kamishna wa sensa Bi. Hajjat Amina Mrisho.

Baadhi ya viongozi wa dini wanaoendelea na mkutano wao jijini Dar es salaam wakipitia vitabu na vipeperushi  vyenye jumbe mbalimbali  kuhusu zoezi la sensa ya watu na makazi litakalofanyika nchi nzima mwezi  Agosti mwaka huu  baada ya wataalam kutoka  Ofisi ya Taifa ya Takwimu kutoa semina fupi kuhusu ushiriki wa viongozi hao katika kufanikisha sensa hiyo 
 
Na Aron Msigwa MAELEZO

No comments:

Post a Comment