Thursday, June 21, 2012

Wazee Kata Ya Kahororo Manispaa Ya Bukoba Wazindua Tawi La Saidia Jamii Ya Wazee Kagera (SAJAWAKA)

 Moja ya kitambulisho walivyopatiwa wazee wa kata ya Kahororo Katika Manispaa ya Bukoba ambavyo vitawasaidia kupata huduma ya Matibabu Bure pamoja namambo mengine ya wazee
 Wazee wa kata ya kahororo wakiwa wanasubiri kufunguliwa kwa tawi lao la SAJAWAKA
 Mwenyekiti wa tawi la saidia Jamii Ya wazee Kagera tawi la Kahororo Silivandi Muyoza akitoa utambulisho kwa wazee
 Wakisoma hotuba yao kwa wageni waliofika katika ufunguzi wa tawi la SAJAWAKA
 Anajulikana kama Mrisho Juma ambaye ni afisa maendeleo ya jamii katika Manspaa ya Bukoba hapa yupo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa
 Vitambulisho vikigawiwa kwa wazee wa kata ya Kahororo katika ufunguzi huo

 Mwenyekiti wa Saidia Jamii Ya Wazee Kagera (SAJAWAKA) Mchungaji Temalirwa akitoa ufafanuzi kwa wazee wa kata Kahororo Manispaa ya Bukoba
 Wakionyesha Vitambulisho vyao kwa mpiga picha wetu

 Hatimae burudani ilianza ama kweli wazee walisakata mziki hadi nilishangaa nilidhani ni vijana kumbe wazee




Bukoba

WAZEE wamashauriwa kutojihusisha na masuala ya siasa na badala yake watafute mbinu mbadala ya kujikwamua kimaisha ili kukabiliana na hari ya ugumu wa maisha ili kuhepuka na suala la kuwa ombaomba katika maisha yao ya kila siku.

Ushauri huo umetolewa na afisa maendeleo ya Jamii Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera Mrisho Issa kwaniaba ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo wakati wa kufungua tawi la Saidia Jamii ya wazee Kagera(SAJAWAKA)  tawi la kata ya Kahororo katika manispaa hiyo ambalo limeanzishwa kwa ajili ya kusaidia wazee.

Alisema kuwa wazee wanapofungua vikundi kama cha (SAJAWAKA) wajue malengo yake na wala wasijihusishe na masuala ya siasa kwani wakati  wa kushabikia  mambo ya siasa uwe nje ya vikundi ambavyo vinatambulika kisheria.

Aliongeza kuwa vipo vikundi vingi vinaanzishwa lakini malengo ambayo wanakuwa wamakusudia luyafanya hawayafanyi na badala yake wanajikuta wameanza kushabikia mambo ya kisiasa nalengowanalokuwa wamekusudia kulifanya halifanyiki.

Katika hatua nyingine alisema kuwa pamoja na kufungua tawi la wazee bado kuna changamoto kwa wazee kutopata huduma ya afya bure hasa wale wanao anzia umri wa miaka 60 na kuendelea kama sera ya wizara husika inavyosema.

Aliongeza kuwa Hospitari nyingi bado jambo hilo hawalitilii maanani na kusababisha usumbufu kwa wazee ambao uwezo wao ni mdogo na kujikuta hawapati huduma ya matibabu bure .

Nae Mwenyekiti wa tawi la Saidia jamii ya wazee Kagera tawi la kata kahororo Silivandi Muyoza alisema kuwa kikundi hicho kina jumla ya wazee 104 na wanatarajia wapewe matibabu bila kudaiwa changizo za tiba kama sra ya wizara ya afya inavyosema na wamepatiwa vitambulisho maalumu vya Chama cha wazeeTanzania (CHAWATA).

Aliongeza kuwa wazee wanatarajia pia kutolipa kodi za viwanja na nyumba zao zisizozalisha biashara kama mwanzo ambapo waliwa wakilipa kodi hizo huku wengine wakiwa na uwezao mdogo.

Aidha alisema kuwa kikundi hicho hakikuanzishwa kwa lengo la siasa na badala yake ni kwa ajili ya kusaidia wazee kimaendelea kwa kubuni mirani mbalimbali ya kuwasaidia katika umri wao wa uzeeni.

Mwisho


No comments:

Post a Comment