Friday, June 15, 2012

Star Yatua Maputo Kuivaa The Mambas





Kocha Kim Paulsen akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Shamim Nyanduga mara baada ya timu hiyo kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Maputo




Kocha Kim Paulsen akiwaongoza wachezaji wake baada ya kushuka kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa maputo jana, nchini Msumbiji. Taifa Stars itakipiga na timu ya Msumbiji The Mambas Jumapili, katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la mataifa ya Afrika zitakazofanyika nchini Afrika Kusini mwaka ujao.


Taifa Stars imewasili Maputo saa 5 asubuhi kwa saa hapa tayari kwa mechi dhidi ya Msumbiji (The Mambas) na kupokewa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Maputo na Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Balozi Nyandugu.


Stars yenye kikosi cha wachezaji 20 chini ya Kocha Mkuu Kim Poulsen imefikia Hotel 2010 LDA iliyoko karibu na Uwanja wa Taifa Zimpeto ambapo mechi hiyo itachezwa Jumapili kuanzia saa 9 kamili kwa saa za hapa ambapo Tanzania itakuwa saa 10 kamili.


Kwa mujibu wa programu ya Kocha Kim, timu itafanya mazoezi leo na kesho katika muda ule ule wa mechi ya Jumapili ambayo itachezeshwa na waamuzi kutoka Madagascar. Mpaka timu inawasili hapa hakuna mchezaji yeyote mwenye matatizo ambayo yanaweza kusababisha asicheze mechi ya Jumapili.



Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Maputo
+258840669404

No comments:

Post a Comment