Friday, June 15, 2012

Usiku Wa Kuamkia Ijumaa


Rais Mstaafu wa awamu ya Mzee Ali Hassan Mwinyi akimkabidhi Mchezaji bora wa mwaka kutoka timu ya Simba na Taifa Stars Shomari Kapombe tuzo yake ya mwanamichezo bora wa mwaka wa  katika tuzo za  zinazoandaliwa na chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA  na kudhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti zilizofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa  Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.

Shomari Kapombe pia amezawadiwa kitita cha shilingi milioni 12 kutoka kwa wadhamini wa tuzo hizo kampuni ya bia ya Serengeti kutokana na ushindi huo wa tuzo ya mwanamichezo bora wa mwaka
Shomari Kapombe mchezji bora wa mwaka akiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa tuzo hizo pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Simba huku akiwa ameshikilia tuzo yake na mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 12 za kitanzania  kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa Serengeti Richard Wells, kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano SBL Teddy Mapunda na wa pili kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Simba Geofrey Nyange Kaburu

Mzee Ali Hassan Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa zamani wa timu ya taifa iliyofanikiwa kushiriki mashindano ya kombe la mataifa huru ya Afrika mwaka 1980 mara baada ya kuwakabidhi tuzo ya heshima usiku wa kuamkia leo
Mzee Ali Hassan Mwinyi akizungumza na kutoa nasaha zake katika utozji wa tuzo hizo.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Kampuni ya bia ya Serengeti SBL Teddy Mapunda akitoa shukurani zake mara baada ya kukamilika kwa utoaji wa tuzo hiyo usiku wa kuamkia leo.
Baba mwenye uzao wa mabondia Mzee Matumla kulia  akikabidhi tuzo ya mwanamchezo bora wa kigeni katika soka Emmanuel Okwi kwa Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Simba Geofrey Nyange aliyepokea tuzo hiyo kwa niaba ya mchezaji huyo,
Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji la Zanzibar ZBC Omar Said Ameir akikabidhi tuzo ya mchezaji bora wa Tanzania katika soka Agrey Morris katika hafla hiyo.
Mchezaji wa zamani wa timu ya Coast Union ya Tanga na Timu ya taifa Salim Amir akikabidhi tuzo kwa mchezaji Shomari Kapombe
Mpiga picha wa siku nyingi Athmani Hamisi akikabidhi tuzo kwa mchezaji bora wa kiume katika mchezo wa VoliboMbwana Ally huku akisaidiwa na msaidizi wake

Mwenyekiti wa kamati ya Tuzo za TASWA Masoud Saanane akizungumza katika hafla ya utozi wa tuzo hizo usiku huu kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee.
Mkurugenzi wa kampuni ya bia ya Serengeti Bw. Richard Wells akizungumza katika hafla ya utoaji wa tuzo za

No comments:

Post a Comment