Wednesday, September 12, 2012

TCCIA Kagera Yakutana Na Waranya Biashara



Afisa wa mamlaka ya mapato mkoani Kagera, Lufungu Mtafya akitoa elimu kwa wafanyabiashara wa manispaa ya Bukoba wanatumia mashine zinazoisaidia mamlaka hiyo kukusanya ushuru, semina ilifanyika kwenye ukumbi wa chama cha msalaba mwekundu na iliandaliwa na TRA kwa kushirikiana na chama cha wafanyabiashara, wakulima na wenye viwanda nchini (TCCIA).



Meneja wa TRA Kagera Leonard Shija kushoto na meneja wa SUMATRA wakisikiliza kwa makini elimu yaliyokuwa inatolewa kwa walipa bodi wanaotumia mashine kukusanya ushuru wa serikali.




Mkurugenzi wa kampuni ya Bukoba Machinery, Rose Kagilita inayojihusisha na uwakala wa ndege ya precision na mataili alikuwa pia miongoni mwa washiriki wa semina, kulia ni diwani wa kata ya Hamgembe Robert Katunzi maarufu kwa jina la tabu gani mara moja.




Baadhi ya viongozi walioandaa semina ya wafanyabiashara wanaotumia mashine za kukusanya ushuru, kutoka kushoto ni Katibu wa TCCIA Rwiza, Meneja wa TRA mkoani Kagera, Leonard Shija na kulia ni meneja wa SUMATRA, Japhet Ole Roysimaye.



Mhasibu mkuu wa kiwanda cha kusindika kahawa kilichoko mkoani Kagera TANICA Joston Rwiza, alikuwa miongoni mwa walioudhuria semina hiyo.




Mwanasheria wa kujitegemea Bw. Chamani alikuwa miongoni mwa walioudhuria semina hiyo.




Baadhi wa wafanyabiashara walioudhuria semina iliyoandaliwa na TRA kwa kushirikiana na TCCIA.

No comments:

Post a Comment