Tuesday, September 18, 2012

Picha Mbalimbali za Wiki Ya Nenda Kwa Usalama Barabarani Bukoba




Wasanii wa kikundi cha sanaa cha KAKAU wakitumbuiza wakati wa ufunguzi wa sherehe za maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama yaliyofunguliwa na mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe kwenye uwanja wa michezo wa Kaitaba.




Baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Kagera wakiwa ndani ya uwanja wa kaitaba wakisubili ufunguzi wa sherehe za maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama.




Massawe akionyeshwa kifaa kinachokagua ubora wa mataili.




Massawe akiwa amesimama wakati akipokea maandamano.




Massawe, akipewa maelezo na PC Fadhil juu ya kifaa kinachodhibiti mwendo kasi.




Mkuu wa mkoa wa Kagera akisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na PC Alexander juu ya alama za barabara.




PC Alexander ambaye ni mkaguzi wa magari wa kitengo cha usalama barabarani mkoani Kagera akimuelezea Massawe mambo yanayohusiana na alama za barabara.




Baadhi ya magari yakiingia kwenye uwanja wa michezo wa kaitaba wakati wa uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama.




Waendesha pikipiki wakiandamana wakati wa uzinduzi wa wiki ya usalama barabarani.

No comments:

Post a Comment