Wednesday, September 19, 2012

Marekani Yatoa Dola Milioni 1 Kuisaidia Tanzania Kuimarisha Mfumo Wa Ulinzi Baharini.



Serikali ya Marekani imetoa msaada wa kuimarisha Mfumo wa Ulinzi baharini wenye thamani ya dola za Marekani milioni 1 ikiwa ni mafunzo pamoja na vifaa.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenhardt ameshiriki katika hafla ya kukata utepe wa kufungua mafunzo pamoja na msaada huo katika kambi ya Kigamboni Wanamaji ya Kigamboni ya TPDF jijini Dar es Salaam.
Msaada huo kwa ujumla utasaidia ushirikiano wa kupata taarifa miongoni mwa Mamlaka za Bandari, askari wa majini na Jeshi la Wananchi wa Tanzania ikiwa ni kuongeza usalama majini.
Picha kwa hisani ya Moblog

No comments:

Post a Comment