Thursday, September 13, 2012

Picha Mbali Mbali




Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabian Massawe akishiriki kwenye zoezi la usafi katika manispaa ya Bukoba.




Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba Khamis Kaputah akimueleza Kanali Massawe mikakati ya kuliondoa dampo la Kashai.




Massawe akiangalia dampo la lililoko eneo la Kashai.



Dampo lililoko kwenye maeneo ya soko la Kashai.




Vijana wakimshangilia Massawe 




7146 Waziri Mkuu, Mizengo Pindanda na Mkewe Tunu (kushoto) wakivuka katika Pantoni ya MV Ujenzi kutoka Kisorya hadi Rugezi Ukerewe wakiwa katika ziara ya mkoa wa Mwanza Septemba 11, 2012. Aliyekaa kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarest Ndikilo na kushoto kwake ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mwanza, Clement Mabina. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Abiria wakisafiri na mizigo yao kati ya Rugezi wilayani Ukerewe na Kisorya wilayani Bunda, Septemba 11, 2012. Ingawa serikali imenunua kivuko kipya chenye uwezo wa kubeba abiria, mizigo na magari bado badhi ya watu wanalipa nauli na kusafiri kwa mitumbwi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)




Basi lenye namba za usajili T329 AMD likiwa limesheni mizigo kuliko uwezo wake likielekea Itigi. Basi hilo lilikuwa likisafiri katika barabara ya Tabora-Itigi-Manyoni mwishoni mwa wiki iliyopita kama lilivyokutwa karibu na stesheni ya reli ya Kazi-Kazi. (Picha na Irene Bwire)



Wamachinga wakiuza bidhaa mbalimbali kwenye mtaa ulioko kwenye barabara ya kuelekea hospitali ya kuu mkoa wa Kagera, halmashauri ya manispaa ya Bukoba ilishawahi kuwapiga marufuku wanachinga kuuza bidhaa zao kwenye eneo hilo, pamoja na amri hiyo wamachinga wameanza kurejea kimyakimya kwenye eneo hilo na kuendelea na biashara yao.




Wanachinga wakiuza bidhaa zao kwenye maeneo yalizuiliwa.




Usafi unaoonekana kwenye barabara za halmashauri ya manispaa ya Bukoba zinatokana na jitihada za Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe, inayoonekana ni barabara ya Kashozi.




Mtaa wa Hoteli ya Lwabizi Plaz



Mamdhari ya mitaa ya halmashauri ya manispaa ya Bukoba.




Barabara ya kuelekea mtaa wa Kashenyi uliko katika kata Kashai ambayo ilikuwa inapitika kwa shida sasa manispaa ya halmashauri ya Bukoba imeanza kuifanyia ukarabati wa kina.




Sehemu ya barabara ya Kashenye

No comments:

Post a Comment