Tuesday, July 24, 2012

Matukio Mbalimbali Mjini Bukoba


Hali hii inaonyesha kwa jinsi gani basi la Sumry ambalo hufanya safari zake kati ya miji ya Dar es salaam na Kagera linavyowapa usumbufu waendesha vyombo vya moto, katika hali ya kawaida basi la sumry uegeshwa katika eneo hili la ushahilini kwenye eneo ya barabara, eneo hili hutumiwa na wamiliki wa basi hili katika kupakia na kupakia abiria tofauti na mabasi mengine ambayo hufanya shughuli maeneo ya standi kuu ya mabasi, hali hii inawapa usumbufu mkubwa watumiaji wa barabara linapoegeshwa basi la Sumry, kama mnavyoona.



Maegesho yasiyo rasmi yaliyoko eneo la uswahilini lililoko katika manispaa ya Bukoba karibu na Q Bar yanayotumiwa na basi la Sumry ambayo sio rasmi.



Baadhi ya wajumbe wa kamati inayoratibu shughuli za kukusanya maoni yaa uundwaji wa katiba mpya, kamati hiyo kwa sasa inakusanya maoni katika manispaa ya Bukoba, hapa inakusanya maoni maeneo ya uwanja wa uhuru.



Waliojitokeza kutoa maoni wakiwa kwenye mstari wakijiandaa kuelezea mapendekezo yao.



Mmoja wa wakazi wa manispaa akitoa maoni.



Baadhi wya wakazi wa manispaa ya Bukoba wakisikiliza mapendekezo yaliyokuwa yakitolewa ya uundwaji wa katiba mpya ya jamhuri.

No comments:

Post a Comment