Monday, July 9, 2012

Matukio Mabilimbali


Walemavu wanaounda kikundi cha BUDAP wakimuonyesha Massawe bidhaa za kazi ya mikono wanazozitengeneza.




Mkuu wa mkoa wa Kagera kanali mstaafu Fabian Massawe, akiwa ndani ya studio ya kituo cha radio cha Kasibante kilichoko mkoani Kagera lililokuwa kwenye viwanja vya maonyesho ya sabasaba yaliyofanyika ndani ya jengo la Chama Cha Mapinduzi (CCM).




Massawe alipotembelea banda na mganga maarufu wa tiba za asili nchini Yustace Nyakubah



Mkuu wa wilaya ya Bukoba kushoto Ziporah Pangani alikuwa mmoja wa walioudhuria sherehe za kilele cha sikukuu ya sabasaba.




Massawe, akisakata ngoma ya Kiganda maarufu kwa jina la Mbutu nyuma yake ni kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera Philip Kalangi.



Kikundi cha waganda kikitumbuiza wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya sabasaba iliyoadhimishwa mkoani Kagera kwenye jengo la Chama Cha Mapinduzi (CCM).



Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimkabidhi zawadi ya balozi wa Ubelgiji nchini aliyemaliza muda wake, Bw. Paul Jansen ambaye alikwenda kuaga, ofisini kwa Waziri Mjini Dodoma Julai 9,2012.(picha na Ofisi ya Waziri Mkuu



Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwasha trekta wakati alipozindua kampeni ya kimkoa ya matumizi ya matrekta makubwa katika kilimo mkoa wa Ruvuma iliyofanyika kwenye uwanja wa zimamoto mjini Songea Julai 7, 2012.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mheshimiwa Kanali Mstaafu Fabian I. Massawe Akiongea na Balozi wa Uingereza Bi Diane Corner na Ujumbe Wake Mara Baada ya Kuwasili Mkoani Kagera na Kufika Ofisini Kwake Kumsalimia.

No comments:

Post a Comment