Saturday, July 6, 2013

CHADEMA YAITISHA KIKAO CHA KAMATI KUU

chadema-logo-i2 493adKAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana katika kikao cha dharura kwa siku mbili mfululizo, kuanzia tarehe 6-7 Julai, 2013, jijini Dar es Salaam.
Katika muda huo wa siku mbili, kikao hicho kitajadili masuala mbalimbali, ambapo agenda zitakuwa; Rasimu ya Katiba Mpya, taarifa ya hali ya siasa nchini, taarifa juu ya mfumo wa uendeshaji wa chama kwa kanda (uzinduzi) na taarifa juu ya uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 26, uliofanyika Juni 16, 2013.
Kupitia agenda za kikao hicho, Kamati Kuu ya CHADEMA, itajadili, kuazimia na kutoa msimamo wa chama juu ya masuala ya kitaifa na mengine yanayohusu maeneo mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya kufanikisha moja ya malengo ya chama ambayo ni pamoja na kutoa uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganaizesheni thabiti kwa ajili ya maendeleo endelevu ya jamii nzima ya Watanzania
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari.
hdg

No comments:

Post a Comment