Monday, December 16, 2013

WANAOCHANGIA KUUENEZA UGONJWA WA UNYANJANO KUKIONA CHA MOTO

 Baadhi ya waandishi wa habari mkoani Kagera wakibadilishana mawazo.
 Ndizi ambayo haijakumbana na ugonjwa wa mnyauko maarufu kwa jina la unyanjano.
 Migomba ambayo haijaathirika.
 Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe, wa pili toka kulia akiwa na baadhi ya watafiti wa kituo cha utafiti wa mazao cha Maruku.

 Mkuu wa mkoa wa Kagera, Kanali Mstaafu Fabian Massawe ameziagiza halmashauri za wilaya na manispaa katika mkoa wa Kagera kutunga sheria ndogo ndogo zitakazowabana wakulima wanaochangia kueneza ugonjwa wa unyanjano.

Ametoa agizo hilo mara baada ya kutembelea shamba la mkulima bora wa ndizi lililopo eneo la mwanzo mgumu katika wilaya ya Misenyi, amesema ugonjwa wa unyanjano unathibitiwa, amewaambia wakulima watumie mbinu bora za kilimo za kuuzuia ugonjwa huo unaoenea kwa kasi katika maeneo mbalimbali mkoani Kagera.

Amewaambia viongozi kuanzia ngazi ya kata hadi mkoa kuwafikisha mahakamani wakulima wote ambao watakuta migomba yao imeathirika, pia ameahidi kuwawajibisha watendaji wote wa serikali ambao watashindwa kusimamia zoezi la kuthibiti uginjwa wa mnyauko.
Baadhi ya watafiti, kulia Bw. Sayi Bulili na kushoto nbi Bw. Leonard Mkandala.

No comments:

Post a Comment