Wednesday, February 27, 2013

RAIS KIKWETE ATEMBELEA JKT

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na uongozi wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jijini Dar es salaam alipotembelea leo February 27, 2013. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange pia walihudhuria.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jijini Dar es salaam alipotembelea leo February 27, 2013. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange pia wapo.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea zawadi ya saa toka kwa  Mkuu  wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Raphael Muhuga huku  Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange wakishuhudia. Saa hiyo imeandaliwa na makamanda wa JKT kumpongeza Rais Kikwete kwa kurejesha mafunzo ya jeshi la ulinzi kwa mujibu wa sheria kuanzia mwaka huu.

UZINDUZI WA MPANGO GSI

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikata utepe kuashiria uzinduzi  wa Mpango  Mkakati  wa Miaka Mitano  wa Taasisi  ya  GSI Tanzania  kwenye ukumbi wa hoteli ya Blue Pearl  jijini Dar es salaam Februari 27, 2013. Wapili kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dr.Abdallha Kigoda. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Joyce Mapunjo.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama mikoba katika maonyesho yaliyoambatana na Uzinduzi wa  Mpandgo Mkakati wa Miaka  Mitano wa Taasisi  ya GSI Tanzania kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl jijini Dar es slaam Februari  27, 2013. Kushoto ni Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko, Abdallah Kigoda na kulia ni  Katibu  Mkuu wa Wizara hiyo, Joyce Mapunjo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Tuesday, February 26, 2013

MANDHALI YA CHAMA CHA MSINGI MWEYANJALE KINACHOUNDA KCU 1990 LTD

 Jengo la chama cha msingi cha Mweyanjale kinachojihusisha na kilimo cha kahawa hai 'organic coffee' kinachounda chama cha ushirika Kagera (KCU 1990 LTD).
 Mwenyekiti wa chama hicho, Leopord Mtalemwa akiwa nje ya jengo la chama hicho.
 Maeneo yanayozunguka chama hicho.
Mtalemwa akiongea na waandishi wa habari.

Monday, February 25, 2013

NDANI YA MANISPAA YA BUKOBA KWAWAKA MOTO

MANISPAA ya Bukoba hapakaliki, hii inafuatia hatua ya madiwani wa manispaa hiyo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kususia kikao chama hicho ambacho hufanyika kabla ya kikao cha baraza la madiwani.


Baadhi ya madiwani wa CCM wamesusia kikao hicho baada ya watu wasiofahamika kusambaza waraka unaowakashfu.


Waraka huo unawakashfu madiwani kumi ambao ni pamoja na madiwani wa CCM 8 na wa vyama vya vya upinzani vinavyowaunga mkono 2.


Mwandishi wa waraka huo anatoa kashfa nzito kwa madiwani waliosaini waraka wa kutaka Mstahiki Meya wa manispaa ya Bukoba Anatory Amani apigiwe kura za kutokuwa na imani naye kufuatia tuhuma mbalimbali zinazomkabili.


Baadhi ya madiwani waliiongea walidai mgogoro ulioko kati ya Meya huyo na madiwani kuwa umeishaigawa CCM, kwa anyakati tofauti walisema kuwa hawana imani na meya huyo na ndio maana wanataka kumng'oa.


Walisema kuwa hata kama nyaraka zikisambazwa na kuwakasfu kamwe hawatarudi nyuma, "tunajua waraka huu aliyeuandaa hivyo hatuna wasiwasi nao, moto wetu uko palepale wa kumuondoa Amani madarakani" walisema bila kutaka majina yao yatakjwe.

Walisema kuwa hawataki kuongozwa na kiongozi yoyote mwenye huruka ya ufisadi ambaye anabuni miradi mingi kwa maslahi yake binafsi," Kiongozi yoyote atakayekuwa na mlengo wa kutaka kuifilisi manispaa tutakula naye sahani moja" walimaliza.


Manispaa ya Bukoba sasa kumewaka moto, pande zote zinazopingana kila mmoja anijiona ni mbabe, pande zinazopingana moja unaundwa na kundi la waziri wa maliasili na utalii, Balozi Khamis Kagasheki na upande nyingine inaongozwa ana Meya wa manispaa ya Bukoba Anatory Amani.

Kambi ya Kagasheki inamtaka Meya wa manispaa ya Bukoba Amani anga'atuke na kambi ya Amani inapinga mapendekezo hayo.



WAZIRI PINDA AKUTANA NA BALOZI WA CANADA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akisalimiana na Balozi wa Canada nchini, Mhe.Alexandre Leveque kabla ya mazungumzo yao, Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Februari 25, 2013. (Picha na Ofisi a Waziri Mkuu)

VIONGOZI WASAINI MPANGO WA AMANI WA UMOJA WA MATAIFA

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maal: umu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini  Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 24, 2013
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe Ban Ki-moon akiweka saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maal: umu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini  Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 24, 2013

No comments:

Post a Comment