Tuesday, August 21, 2012

Matukio Mbalimbali


Katibu tawala wa mkoa wa Kagera, Nassor Mnambila akifungua kikao cha kuhamasisha masuala ya sensa na makazi kilichoandaliwa na halmashauri ya manispaa ya Bukoba kwa kushirikiana na wilaya ya Bukoba kilichowashirikisha viongozi wa madhehebu ya dini, viongozi wa vyama vya siasa na waandishi wa habari kilichofanyika kwenye ukumbi wa manispaa ya Bukoba, alikuwa akisema kuwa serikali haitawavumulia wale wote watakaokataa kuhesabiwa.




Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba Robert Kwela Kushoto na katibu tawala wa wilaya ya Bukoba Clement Ndyamkama kulia wakiwasikiliza kwa makini viongozi waliokuwa wanahamasisha masuala ya sensa na makazi.




Mkuu wa wilaya ya Bukoba akiwaeleza viongozi wa dini, waandishi wa habari na viongozi wa vyama vya siasa wawahamasishe wananchi washiriki kikamilifu kwenye zoezi la sensa wa watu na makazi.



Katibu wa Chama Cha Mapinduzi akiongea na wajumbe wa kikao cha kuhamasisha masuala ya sensa.




Baadhi ya waandishi walioudhuria mafunzo ya habari ya uchokonozi wakimskiliza Phil Karashani.




Baadhi ya waandishi wakijadili mambo kwenye makundi.



Baadhi ya waandishi walioudhuria mafunzo ya kuandika habari za uchokonozi wakijadili mambo kwenye makundi.




Phil Karashani akitoa elimu kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Kagera juu ya habari cha uchokonozi.

No comments:

Post a Comment