Wednesday, June 20, 2012

Rais Kikwete akutana na Viongozi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na shirika la nyumba mjini Dodma


Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mkutano na viongozi wa mifuko ya hifadhi ya Jamii na Shirika la Nyumba la taifa ikulu mjini Dodoma leo.Katika kikao hicho Mheshimiwa Rais aliwapa changamoto viongozi hao  kuunganisha nguvu na kubuni mikakati itakayowezesha kuwapatia watumishi wa umma nyumba za kuishi. PICHA NA FREDDY MARO
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisisitiza jambo wakati akiongea na mkurugenzi mkuu wa PPF Bwana William Eriyo mjini Dodoma leo baada ya kikao maalumu na viongozi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na shirika la Nyumba .
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na shirika la Nyumba la Taifa mara baada ya kikao maalumu kilichofanyika ikulu mjini Dodoma leo. viongozi Wengine waandamizi w aliohudhuria kikao hicho Naibu Waziri wa Ardhi Goodluck ole Medeye(watatu kushoto),Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue(Wanne kushoto),Gavana wa Benki Kuu Professa Beno Ndulu(kulia) na naibu katibu Mkuu Hazina Dr.Servacius Likwelile(kushoto). Katika kikao hicho Mheshimiwa Rais aliwapa changamoto viongozi hao  kuunganisha nguvu na kubuni mikakati itakayowezesha kuwapatia watumishi wa umma nyumba za kuishi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Bwana Nehemiah  Mchechu mara baada ya kikao maalumu kilichofanyika ikulu mjini Dodoma leo(picha na Freddy Maro)
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dr.Ramadhani Dau akiteta Jambo na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu mjini Dodoma jana.

No comments:

Post a Comment