Saturday, April 21, 2012

Kilimo Cha Migomba Kuboreshwa Kagera

 Mratibu wa Mradi wa migomba unaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania na Ubeligiji Mgenzi Byabachwezi akitoa maelezo ya jinsi ya kudhibiti magonjwa yanayoshambulia migomba kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe alipotembelea shamba la kikundi cha Mshikamano Kata ya Magoma Wilayani Ngara wiki hii. PICHA NA PHINIAS BASHAYA
Na.Kibuka Prudence,Ngara
 
Shirika la Maendeleo la Ubeligiji(BTC)kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania limetumia zaidi ya shilingi bilioni 120 kwa ajili ya mradi wa migomba unatekelezwa katika wilaya zote za Mkoa wa Kagera na Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma.
Hayo yamebainishwa na Afisa Miradi shirika hilo hapa nchini Cranme Chiduo, wakati wa maadhimisho ya siku ya zao la ndizi yaliyofanyika katika kijiji cha Rusumo wilayani Ngara ambayo yamefunguliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massaawe.
Amesema tangu Mradi wa BTC yaani (Belgium Technical Corporation)  uanzishwe miaka minne iliyopita mbali na kutumia kiasi hicho cha fedha pia umepata mafanikio makubwa katika usambazaji wa mbegu bora za migomba na kuwasaidia wasindikaji na wasambazaji kuongeza thamani ya zao la ndizi.
Katika maadhimishisho hayo Mratibu wa Mradi wa Migomba Mkoani Kagera Mgenzi Byabachwezi alisema hadi Desemba mwaka jana zaidi ya miche bora ya migomba milioni mbili imesambazwa kwa wakulima 46,000 katika maeneo unapotekelezwa mradi huo.
Pia alisema mradi huo unaogharamiwa na Serikali za Ufalme wa Ubeljiji naTanzania,ulianza kutekelezwa tangu mwaka 2009 kwa sambaza miche ya migomba ambao umeweka mwamko endelevu wa kusindika mazao ya migomba na utaalamu wa masoko.
Akizindua maonyesho hayo Mkuu wa Mkoa wa Kagera aliwataka wakulima wa migomba kuachana na kilimo cha mazoea na kuelekeza nguvu kwenye kilimo cha biashara.
Aidha,Massawe alitaka wakulima wapewe elimu ya ujasiliamali ili kujipatia ujuzi ambao pia utawasaidia kupeleka mazao yao kwenye masoko wao wenyewe bila kutegemea walanguzi wa mazao yao.
Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa wa Kagera aliwaomba wafadhili wa Mradi huo kuanzisha pia maadhimisho ya zao la mgomba katika mikoa mingine nchini inayolima zao hilo.
Katika maadhimisho hayo Massawe pia aliiasa jamii kuachana na tabia ya utegemezi wa wafadhili na kuwa baada ya kusaidiwa katika hatua za awali tunalazimika kujitegemea wenyewe.
Mwisho



No comments:

Post a Comment