Thursday, April 11, 2013
Dodaoma Wiki Hii
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid (kulia) , Mbunge wa Kilindi Beatrice Shellukindo (Wapili kulia) na Mbunge wa Viti Maalum, Zainab Kawawa kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma, Aprili 10, 2013.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mbunge wa Viti Maalum, Zarina Madabida wakitoka kwenye ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma, Aprili 10, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
MAELEZO YA ZITTO KABWE KUHUSU BARUA ALIYOMUANDIKIA SPIKA MAKINDA
"Nimeandika barua Kwa Spika wa Bunge kutaka Waziri wa Nishati na Madini
kutoa maelezo Bungeni kuhusu uamuzi wake wa kuwapa leseni kubwa ya
kuchimba #Uranium huko wilayani Namtumbo. Mnamo tarehe 10 Agosti 2012
Waziri alitamka ndani ya Bunge "sisi tunajua zaidi ya anavyojua yeye,
Leseni haijatolewa na haitatolewa mpaka Kampuni ya #MantraResources
ilipe kodi".
Kodi ya ongezeko la mtaji (capital gains tax) ya $189m kufuatia mauzo ya mradi wa #MkujuRiverProject kutoka kampuni ya Mantra kwenda kampuni ya AMRZ ya Urusi iligomewa kulipwa. #TRA wamepeleka shauri hilo mahakama ya kodi na mpaka sasa maamuzi hayajatolewa. Kwa mujibu wa mabadiliko ya Sheria ya mwaka 2012, kabla ya Waziri mwenye dhamana ya madini kubariki mauzo ya kampuni, anapaswa kupata Kibali Cha kwamba kodi zote stahili zimelipwa. Kibali Kwa kampuni ya mantra kilitolewa bila kujali hitaji la kisheria na sasa kampuni hii imepewa leseni.
Maamuzi haya ya Waziri wa Nishati na Madini yanalikosesha Taifa mapato ya zaidi ya tshs 300bn ambazo zingeweza kumaliza tatizo la nyumba za walimu nchi nzima na kulipia madai yote ya walimu. Fedha hizi zingeweza kujenga barabara ya lami kutoka Manyoni mpaka Itigi. Fedha zingeweza kukarabati reli ya Kati na kuirejesha katika ubora wa unaotakiwa. Kwa mujibu wa kanuni za Bunge nimetaka Waziri atoe maelezo bungeni na wabunge wajadili. Ni dhahiri kwamba serikali inayoongozwa na CCM imeamua kumaliza utajiri wote wa nchi na kuugawa Kwa wageni Kwa bei ya Che. Wananchi Ni lazima kusimama imara kukataa uporaji huu na maamuzi haya ya kiburi Cha kudharau Bunge yaliyoyafanywa na Serikali.
Kodi ya ongezeko la mtaji (capital gains tax) ya $189m kufuatia mauzo ya mradi wa #MkujuRiverProject kutoka kampuni ya Mantra kwenda kampuni ya AMRZ ya Urusi iligomewa kulipwa. #TRA wamepeleka shauri hilo mahakama ya kodi na mpaka sasa maamuzi hayajatolewa. Kwa mujibu wa mabadiliko ya Sheria ya mwaka 2012, kabla ya Waziri mwenye dhamana ya madini kubariki mauzo ya kampuni, anapaswa kupata Kibali Cha kwamba kodi zote stahili zimelipwa. Kibali Kwa kampuni ya mantra kilitolewa bila kujali hitaji la kisheria na sasa kampuni hii imepewa leseni.
Maamuzi haya ya Waziri wa Nishati na Madini yanalikosesha Taifa mapato ya zaidi ya tshs 300bn ambazo zingeweza kumaliza tatizo la nyumba za walimu nchi nzima na kulipia madai yote ya walimu. Fedha hizi zingeweza kujenga barabara ya lami kutoka Manyoni mpaka Itigi. Fedha zingeweza kukarabati reli ya Kati na kuirejesha katika ubora wa unaotakiwa. Kwa mujibu wa kanuni za Bunge nimetaka Waziri atoe maelezo bungeni na wabunge wajadili. Ni dhahiri kwamba serikali inayoongozwa na CCM imeamua kumaliza utajiri wote wa nchi na kuugawa Kwa wageni Kwa bei ya Che. Wananchi Ni lazima kusimama imara kukataa uporaji huu na maamuzi haya ya kiburi Cha kudharau Bunge yaliyoyafanywa na Serikali.
BUNGE LA BAJETI WABUNGE WAPANGUA KANUNI
Spika wa Bunge, Anne Makinda akipitia makabrasha yake wakati akiongoza kikao cha kwanza cha Mkutano wa 11 wa Bunge la Bajeti, Dodoma jana
Dodoma. Baada ya siku mbili za mjadala mzito kuhusu mabadiliko
ya Kanuni za Bunge, jana Bunge limepitisha azimio la mabadiliko
yanayohusu utaratibu wa kutunga sheria kuhusu mambo ya fedha pekee.
Kwa uamuzi huo, mambo mengine ambayo yalikuwa yamependekezwa lakini hayahusiani na sehemu hiyo, yaliachwa baada ya kuibua mjadala mzito na kupingwa na baadhi ya wabunge.
Miongoni mwa mabadiliko yaliyofanyika, muda wa kuchangia hoja kwa wabunge katika Mkutano wa Bajeti unaoendelea umepunguzwa kutoka dakika 15 hadi 10, huku wabunge wakipigwa marufuku kutumia muda wao adhimu kutoa pongezi na pole, bali kuingia moja kwa moja kwenye hoja.
Hayo yaliamualiwa jana bungeni baada ya Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni za Bunge na Naibu Spika, Job Ndugai kuwasilisha azimio la marekebisho ya kanuni za Bunge ambalo lilipitishwa.
Akichangia hoja ya azimio hilo Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu hakutaka muda wa kuzungumza upunguzwe kwa kuwa sehemu hiyo ni sehemu ya mazungumzo na si vinginevyo.
Hata hivyo Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki alikubaliana na pendekezo la kubadili muda kutoka dakika 15 hadi 10 akieleza kuwa litatoa nafasi kwa wabunge wengi kuchangia.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Anna Abdallah alisema mabadiliko hayo yanalipa Bunge uwezo wa kuisimamia Serikali katika mambo ya fedha.Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid alisema dakika 10 ni nyingi na mtu akijipanga vizuri zinatosha kukamilisha hoja zake.
Suala jingine ambalo limefanyiwa mabadiliko ni kuwekwa uwiano wa kuchangia hoja ambapo wabunge sasa watapangwa kulingana na idadi yao kivyama.
Wednesday, April 10, 2013
NCHEMBA;VIDEO YA LWAKATARE NILIIPELEKA MIMI POLISI
Nchemba amekuwa akitajwa na viongozi wa CHADEMA kuwa anahusika kutengeneza video hiyo, kwa kuwa aliwahi kutamba wakati akihojiwa na kituo kimoja cha televisheni kuwa anayo video inayowaonesha viongozi wa chama hicho wakipanga mauaji.
Hata hivyo, tangu Nchemba atoe kauli hiyo Januari mwaka huu, Jeshi la Polisi lilikaa kimya hadi Machi 12 lilipomkamata na kumhoji Lwakatare, siku moja baada ya video hiyo kuwekwa kwenye mtandao wa You tube na mtu anayejiita ‘Bukoba Boy’.
Akizungumza na gazeti hili kwa simu jana, Nchemba alikiri kuwa ndiye aliyeipeleka video ya Lwakatare polisi na kwamba alifanya hivyo baada ya kuripoti kuandikiwa ujumbe wa simu wa kutishiwa maisha na baadhi ya viongozi wa CHADEMA.
“Niliwapelekea mimi hiyo video polisi na wakati nasema kwenye televisheni nilikuwa tayari nimewapa. Na pale nilisema makusudi baada ya Zitto Kabwe kudai kuwa mwaka jana kulitokea mauaji mengi, ndipo nikataka kumuonesha kuwa chama chake kinahusika na mikakati hiyo,” alisema.
Alipoulizwa aliipataje video hiyo na kwanini hajahojiwa polisi ili kutoa uthibitisho wa uhalali wake, Nchemba alisema: “Kuna msamaria mwema aliniletea.”
Nchemba alipobanwa ana uhakika gani kama video hiyo ina ukweli, alijibu kuwa: “Ile huhitaji akili kubwa kutambua uhalisia wake. Suala la Lwakatare CHADEMA wakubali tu na wajitokeze hadharani kwenye makanisa na misikiti, watubu na kuomba radhi kwa umma.”
Hata hivyo katika kile kinachoweza kuongeza mashaka ya Nchemba kuhusishwa kutengeneza video hiyo, alikwenda mbali zaidi akitoa hata siri za polisi, akisimulia maelezo aliyodai kuwa ndiyo yalitolewa na Lwakatare wakati akihojiwa na polisi.
“Pale video inaonesha ni nyumbani kwake, tena jikoni na hilo amekiri katika maelezo yake polisi. Pia amekubali kuwa siku hiyo alipiga chafya kama inavyoonekana. Sasa wewe mwandishi unatetea nini wakati yeye amekiri polisi kila kitu kilichomo mle,” alisema.
Maelezo ya Nchemba yalionekana kumtia hofu mmoja wa mawakili wa Lwakatare, ambaye alikuwepo wakati wote wa mahojiano polisi, Nyaronyo Kicheere, akidai kuwa ni wazi jeshi hilo linafanya kazi ya propaganda za CCM.
“Nchemba hakuwepo wakati Lwakatare akihojiwa na hata baadhi ya wanasheria katika kesi yake ya ugaidi inayomkabili hawajui alichokisema polisi, sasa huyo amepata wapi siri za polisi kama si mchezo unachezwa?” alihoji.
Kuhusu mahusiano yake na mshtakiwa wa pili katika kesi ya Lwakatare, Ludovick Joseph, ambaye anadaiwa na baadhi ya watu kuwa ndiye aliyerekodi video hiyo, Nchemba alisema walifahamiana kupitia mtandao wa kijamii wa facebook.
Alipotakiwa kufafanua ukaribu wao hadi kufikia hatua ya kumtumia fedha kwa njia ya M-Pesa kupitia simu yake, Nchemba alisema: “Mimi nilimtumia kama ninavyowapa watu wengine hata wa CHADEMA.
“Mimi sijui kama Ludovick ndiye alirekodi video hiyo, wala sikuwahi kumtuma kufanya hivyo na fedha niliyomtumia si kwamba nilikuwa nikimlipa ujira. Kwani unaweza kumpa mtu sh 50,000 tu kwa kazi hiyo?” alihoji.
Tanzania Daima lilipotaka kufahamu kama anahusika kushirikiana na vyombo vya dola kuwarubuni baadhi ya vijana wa Makao Makuu CHADEMA kwa fedha ili watumike kutoa ushahidi wa kumwangamiza Lwakatare mahakamani, Nchemba alisema: “CHADEMA haijawahi kuongoza serikali, hivyo hawajui mikono ya serikali.”
Alipotakiwa kufafanua kikao baina yake na vijana hao kilichofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff ya jijini Dar es Salaam mwishoni mwa mwezi uliopita na kisha kuwatumia fedha kwa njia ya M-Pesa, Nchemba aling’aka na kuuliza: “Hiyo Hoteli ya Sea Cliff iko wapi? Maana sipajui na sijawahi kufika.”
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Mkurugenzi wa Mambo ya Katiba wa CHADEMA, Tundu Lissu, alifichua njama zinazofanywa ili kutengeneza ushahidi wa uongo kwa ajili ya kuutumia katika kesi ya ugaidi inayomkabili Wilfred Lwakatare.
Lissu alidai kuwa njama hizo zinafanywa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama na ujasusi ili kutumia ushahidi huo mahakamani dhidi ya Lwakatare.
Alisema kuna baadhi ya vijana wa CHADEMA wa Idara ya Ulinzi na Usalama wanaopewa fedha na kuahidiwa kufundishwa namna ya kuzungumza katika kesi hiyo ya Lwakatare.
Lissu alisema kuna baadhi ya vijana wakiongozwa na Saumu Mulugu, ambaye alifukuzwa kazi CHADEMA mwanzoni mwa mwaka jana, wamepokea fedha kutoka kwa kigogo mmoja wa CCM (jina linahifadhiwa) ili kufanikisha mpango huo.
Lissu alisema hadi sasa vijana hao wameshapewa sh 400,000 ili wakubali kwenda kufundishwa jinsi ya kuzungumza mahakamani kuwa CHADEMA ni chama cha kigaidi, kwamba Lwakatare alipanga mikakati ya kigaidi.
“Awali walipewa sh 400,000, wakapewa tena sh 300,000, pia wakapewa sh 35,000 mara mbili. Na fedha zote hizi walikuwa wanapewa kwa njia ya M-Pesa,” alisema Lissu.
Alidai kuwa Saumu ndiye anayeratibu mpango wote kati ya Jeshi la Polisi na vijana hao wa CHADEMA kwa kuwarubuni kwa fedha.
Alisema vikao baina ya vijana hao wa CHADEMA na Saumu vimewahi kufanyika mara kadhaa katika moja ya hoteli maarufu nchini juu ya mambo ya kwenda kuzungumza kwenye vyombo vya habari au mahakamani kwenye kesi ya Lwakatare.
Siku moja baada ya madai ya Lissu, gazeti hili lilimnasa Saumu akiwa anawasiliana na wenzake, huku akiwatuhumu baadhi yao kuwa ndio waliovujisha siri kwa Lissu.
Vilevile alionekana akiwasiliana na kigogo mmoja wa CCM ambaye alikuwa akimwita ‘mkuu’ huku akimsomea baadhi ya taarifa zilizoandikwa magazetini jana yake kuhusu kuvuja kwa siri zao.
Saumu akiwa katika grosari karibu na baa maarufu kwa jina la Kwa Kimaro, jirani na eneo la Benki Kuu ya Damu Salama, Mchikichini jijini Dar es Salaam, alisikika akiwalalamikia wenzake kwa kumsaliti na kuvujisha mkakati wao kwa Lissu.
“Kwanini mmelikisha siri zetu kwa Lissu hadi amejua tulikutana katika hoteli ya kifahari na Mwigu…? Sasa nitawaonesha, maana laki tano zenu ninazo mimi. Siwapi bali nitazitumia kujilinda,” alitamba.
Saumu ambaye alikuwa akizungumza kwa sauti kubwa ya ghadhabu kupitia simu, aling’aka: “Nyie kwanini mmeniuza kwenye ishu ambayo tumeipanga wote?”
Baada ya kupokea maelekezo kutoka kwa ‘mkuu wake’ aliendelea kupiga simu akimlalamikia mtu ambaye hakumtaja, kuwa alikuwa amezima simu yake makusudi kwa kuwa ndiye alivujisha siri zao kwa CHADEMA.
“Mimi sitakubali na nimehakikishiwa na bosi wetu kuwa huyo aliyetusaliti tutatumia wale askari kumwekea hata unga. Haiwezekani fedha tumepokea za kwanza, za pili na tatu kwanini tuuzane dakika za mwisho?” alidai Saumu huku akiendelea kugida bia yake.
Huku akihaha huku na kule, Saumu alikuwa akiwapigia simu baadhi ya madereva wa CHADEMA makao makuu na kuwaomba simu za baadhi ya watu, na hata wakati mwingine kuwafokea akidai ndio waliofichua siri hiyo.
Hata hivyo, baada ya kutilia shaka nyendo za chanzo chetu kudaka siri zake, ghafla alitokomea na kuzima simu zake mara moja kwani hata alipotafutwa baadaye hakupatikana hadi leo.
Polisi wafanya unyama
Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi nchini limemkamata kada wa CHADEMA mjini Bukoba, Evodius Justinian na kumshikilia kwa siku kadhaa kisha kumsafirisha hadi jijini Dar es Salaam huku akipewa mateso makali ya kulazimishwa akubali kutengeneza video ya Lwakatare.
Justinian (30), ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA) mjini Bukoba, alikamatwa Jumanne ya wiki iliyopita akidaiwa kukabiliwa na makosa ya jinai.
Alishikiliwa kwa siku mbili mfululizo kabla ya kumsafirisha kwenda wilayani Igunga, Tabora ambako alidaiwa kuwa alitenda makosa hayo ya jinai lakini alifichwa jijini Mwanza.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi hakutaka kulizungumzia kwa undani suala hilo lakini aligusia kuwa alikuwa anakabiliwa na mashitaka ya kushambulia na kujeruhi mtu huko wilayani Igunga.
Hata hivyo, kada huyo alisafirishwa hadi uwanja wa ndege wa jijini hapa juzi, lakini akanyang’anywa simu na kukatazwa kuzungumza na ndugu zake.
Taarifa za kada huyo kuletwa jijini hapa zilikuwa za kificho kwani wakili wake Nyaronyo Kicheere akiongozana na ndugu wa mtuhumiwa huyo walifika Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na kuelezwa kuwa amepelekwa makao makuu.
Walipofika makao makuu kumwona na kumpatia chakula, polisi walisema hawana mtu kama huyo, hivyo wakarudi tena Kanda Maalumu walipohakikishiwa kuwa yuko makao makuu.
Akizungumza mbele ya wakili wake, Kicheere, mtuhumiwa huyo alieleza unyama aliofanyiwa na jeshi hilo wakati wote wa mahojiano mkoani Mwanza na jijini hapa.
Katika maelezo yake yaliyoshuhudiwa na Ofisa wa Polisi Makao Makuu, Advocate Nyombi, Justinian alisema kuwa baada ya kutolewa mjini Bukoba kwa siri bila ndugu zake kujua, alipelekwa jijini Mwanza na kuhojiwa bila kuruhusiwa kuonana na wakili wake.
Alieleza kuwa wakati wote wa mahojiano hayo alikuwa akilazimishwa kukiri kurekodi video ya Lwakatare inayoonesha mikakati ya ugaidi.
Alisema alisafirishwa kwa siri kwa ndege hadi Dar es Salaam, akapelekwa chooni na kumpiga, kutishiwa na kuteswa kwa nyaya za umeme na kumnyima fursa ya kupewa chakula.
Justinian ambaye anaendelea kushikiliwa na polisi, anatarajiwa kufikishwa mahakamani leo.
Kabla ya maelezo hayo, Kicheere akiwa na Uloleulole Juma Athumani, ambaye ni ndugu wa Justinian, alijitambulisha kwa Nyombi akimweleza kuwa walikuja kuonana na mteja wake pamoja na kumletea chakula.
Hata hivyo, Nyombi alisema hakuwa na habari za kukamatwa kwa kada huyo na kwamba angekuwa amelimaliza mapema suala hilo.
Kada huyo alisimulia unyama aliofanyiwa akisema: “Nimepigwa na polisi nikiwa Mwanza, nikiwa chooni Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam wakati naletwa huku, polisi wakaniambia mimi ni mtu hatari sana, niseme nilifanya nini Igunga.
“Nikiwa Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam niliomba kwenda chooni, waliingia pamoja na mimi wakanipiga sana, nimeshaandika maelezo kwa kulazimishwa, niliomba kuwa na wakili wakanikatalia,” alisema.
Aliongeza kuwa akiwa Dar es Salaam alihojiwa aseme ukweli kuhusu video ya Lwakatare. Akawajibu kuwa ilifanyiwa uhariri na Ludovick lakini akapigwa makofi na askari wakaagiza nyaya za umeme za kutesea.
“Waliposimama kuleta nyaya za umeme, kwa kuhofia mateso ya umeme nikasema hii video ni yangu. Ninaumwa sana tumbo la kuhara damu, natumia dawa nilizonunuliwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Mkoa wa Kagera tarehe 4 Aprili,” alisema.
Justinian aliongeza kuwa hakula chakula chochote cha polisi kwa kuwa hawaamini, ila kuhara kulipozidi alikubali kula chakula chao.
Wakili Kicheere alisema ni makosa makubwa sana kumtesa mtu kwa kipigo na vitisho vya umeme na kwamba hayakubaliki hata mahakamani.
“Polisi hawakutaka nionane naye kwa makusudi hadi walipomaliza kumhoji na kumtesa ndipo wakaniruhusu,” alisema.
CHANZO:TANZANIA DAIMA
WANAFUNZI WA CHUO KIKUU HURIA KITUO CHA BUKOBA WAKIWA KATIKA MAKUNDI KABLA YA ZOEZI LA FACE TO FACE
Mkurugenzi wa chuo kikuu huria kituo cha Bukoba, Profesa Babyegeya akitoa maelekezo kwa mmoja wa wanafunzi.
Asilimia 26.5 wanawake hufanya mapenzi kinyume na maumbile
Wakati idadi ya wanawake wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ikiongezeka, asilimia 26.5 ya wanawake Tanzania wamebainika kuwa wanafanya mapenzi kinyume na maumbile.
Mfumo wa uzazi unaharibika
Watafiti wanabainisha kuwa kitendo
hicho licha ya ukweli hakifai kwa vile kinaharibu mfumo wa uzazi, kina
athari kubwa mno kwa mwanadamu, mojawapo ni ikiwemo uwezekano mkubwa wa
wahusika kuambukizana virusi vya Ukimwi kwa vile hakuna vilainishi,
hivyo kusababisha michubuko ambayo ndio njia kuu ya kuambukiza vijidudu
hivyo.
Mtafiti Mwanasayansi, Irene Mremi
kutoka Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu nchini
Tanzania (NIMR) alitoa ripoti hiyo hivi karibuni hapa jijini Dar Es
Salaam.
Mremi akiwa na jopo la watafiti kutoka
NIMR anasema kuwa wanawake hao wamesema chanzo kikubwa kinacho
wapelekea kufanya ngono kinyume na maumbile ni kujipatia kipato zaidi na
Kuogopa kupata Mimba.
Vilevile alizitaja sababu nyingine za
wanawake kufanya mapenzi kwa njia hiyo ni kulinda usichana wao na
baadhi ya mila na tamaduni za baadhi ya makabila.
Sampuli za utafiti
Utafiti huo ulikusanya sampuli kutoka katika mikoa ya Dar es salaam, hasa maeneo ya Kinondoni, Tanga, Makete na Siha.
Mremi anasema “Utafiti wetu
uliwahusisha wasichana na wanawake wa rika kuanzia miaka 15 na kuendelea
na kada tofauti katika jamii kama wanafunzi, wafanyakazi, wahudumu wa
bar, wauguzi, makahaba na akina mama wa nyumbani
Katika maeneo hayo watu 903 walijitokeza wakiwepo pia wanaume ambao walihusishwa katika utafiti huo.
Imani potofu kwa wanaume
Wanaume waliohojiwa wamesema wanafanya
kwa ajili ya kupata raha tu na imani ya kuwa huko hakuna maaambukizi ya
VVU, kitu ambacho ni uongo, kwani huko ndiko kwenye kuchangia ukimwi
kwa haraka zaidi kuliko sehemu nyingine yoyote. CHANZO MWANANCHI
AFRICAN Barrick Gold (ABG) has appointed Janet Reuben-Lekashingo as the Organizational Effectiveness Director of ABG.
Janet assumed her position effectively from 1 April, 2013, making her one of the most senior Tanzanians in the mining company.
Her main duties will be to work with the team to lead evolution of the human resources function to Employee Effectiveness Management, ensuring that ABG has all organizational conditions required to utilise the available workforce at their full potential and effectively ensure all the control mechanisms for monitoring the effectiveness of the employee utilisation are in place.
Her last appointment in ABG was Corporate Human Resources Manager, where her main responsibilities included Talent Management and Learning & Development and advising ABG's mine sites on Human Resources related processes.
Janet joined ABG as the Human Resources Manager for the Dar es Salaam office and working with specific projects with the mine sites in October 2008. She has worked in different capacities within the Human Resources Function in the company.
Prior to joining ABG, she was the Human Resources Manager for AngloGold Ashanti's Geita Gold Mine where she started her mining industry career after spending 5 years in the aviation industry.
Janet has a Masters Degree in Arts from the University of Dar es Salaam and a Post Graduate Diploma in Management from the Graduate School of Business at the University of Cape Town.
She is a member of the Society for Human Resource Management (SHRM) as well as an affiliate member of the Chartered Institute of Personnel and Development (CIPD).
Janet was a Board member of the Association of Tanzanian Employers (ATE) for the past six years and is currently a Board Member of the Tanzanian Wage Board.
Tuesday, April 2, 2013
Kamati Kuu Chadema Kukutana Dar
Wednesday, 03 April 2013
Published in Siasa
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana kwa siku mbili kwenye kikao chake cha kawaida jijini Dar es Salaam, kuanzia tarehe 3-4 Aprili, 2013.
Katika kikao hicho cha siku mbili, Kamati Kuu itajadili pamoja na mambo mengine, yatokanayo na kikao kilichopita, hali ya kisiasa nchini, pia itapokea taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha Baraza Kuu kilichofanyika mwezi Februari mwaka huu, ikiwemo mpango wa uendeshaji chama kwa kanda.
Aidha, Kamati Kuu pia itajadili mpango kazi na bajeti ya Chama kwa mwaka 2013-2014
Imetolewa Aprili 2, 2013, Dar es Salaam na;
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari CHADEMA
Wednesday, 03 April 2013
Published in Siasa
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana kwa siku mbili kwenye kikao chake cha kawaida jijini Dar es Salaam, kuanzia tarehe 3-4 Aprili, 2013.
Katika kikao hicho cha siku mbili, Kamati Kuu itajadili pamoja na mambo mengine, yatokanayo na kikao kilichopita, hali ya kisiasa nchini, pia itapokea taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha Baraza Kuu kilichofanyika mwezi Februari mwaka huu, ikiwemo mpango wa uendeshaji chama kwa kanda.
Aidha, Kamati Kuu pia itajadili mpango kazi na bajeti ya Chama kwa mwaka 2013-2014
Imetolewa Aprili 2, 2013, Dar es Salaam na;
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari CHADEMA
Subscribe to:
Posts (Atom)



















