Wednesday, April 10, 2013

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU HURIA KITUO CHA BUKOBA WAKIWA KATIKA MAKUNDI KABLA YA ZOEZI LA FACE TO FACE





Mkurugenzi wa chuo kikuu huria kituo cha Bukoba, Profesa Babyegeya akitoa maelekezo kwa mmoja wa wanafunzi.



Asilimia 26.5 wanawake hufanya mapenzi kinyume na maumbile

3 bfb73
Wakati idadi ya wanawake wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ikiongezeka, asilimia 26.5 ya wanawake Tanzania wamebainika kuwa wanafanya mapenzi kinyume na maumbile.

Mfumo wa uzazi unaharibika
Watafiti wanabainisha kuwa kitendo hicho licha ya ukweli hakifai kwa vile kinaharibu mfumo wa uzazi, kina athari kubwa mno kwa mwanadamu, mojawapo ni ikiwemo uwezekano mkubwa wa wahusika kuambukizana virusi vya Ukimwi kwa vile hakuna vilainishi, hivyo kusababisha michubuko ambayo ndio njia kuu ya kuambukiza vijidudu hivyo.
Mtafiti Mwanasayansi, Irene Mremi kutoka Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu nchini Tanzania (NIMR) alitoa ripoti hiyo hivi karibuni hapa jijini Dar Es Salaam.
Mremi akiwa na jopo la watafiti kutoka NIMR anasema kuwa wanawake hao wamesema chanzo kikubwa kinacho wapelekea kufanya ngono kinyume na maumbile ni kujipatia kipato zaidi na Kuogopa kupata Mimba.
 Vilevile alizitaja sababu nyingine za wanawake kufanya mapenzi kwa njia hiyo ni kulinda usichana wao na baadhi ya mila na tamaduni za baadhi ya makabila.
Sampuli za utafiti
Utafiti huo ulikusanya sampuli kutoka katika mikoa ya Dar es salaam, hasa maeneo ya Kinondoni, Tanga, Makete na Siha.
 Mremi anasema “Utafiti wetu uliwahusisha wasichana na wanawake wa rika kuanzia miaka 15 na kuendelea na kada tofauti katika jamii kama wanafunzi, wafanyakazi, wahudumu wa bar, wauguzi, makahaba na akina mama wa nyumbani
Katika maeneo hayo watu 903 walijitokeza wakiwepo pia wanaume ambao walihusishwa katika utafiti huo.
Imani potofu kwa wanaume
Wanaume waliohojiwa wamesema wanafanya kwa ajili ya kupata raha tu na imani ya kuwa huko hakuna maaambukizi ya VVU, kitu ambacho ni uongo, kwani huko ndiko kwenye kuchangia ukimwi kwa haraka zaidi kuliko sehemu nyingine yoyote. CHANZO MWANANCHI

ABG appoints Janet Reuben-Lekashingo Organizational Effectiveness Director

JANET REUBEN-LEKASHINGO 17984
AFRICAN Barrick Gold (ABG) has appointed Janet Reuben-Lekashingo as the Organizational Effectiveness Director of ABG.

Janet assumed her position effectively from 1 April, 2013, making her one of the most senior Tanzanians in the mining company.
Her main duties will be to work with the team to lead evolution of the human resources function to Employee Effectiveness Management, ensuring that ABG has all organizational conditions required to utilise the available workforce at their full potential and effectively ensure all the control mechanisms for monitoring the effectiveness of the employee utilisation are in place.
Her last appointment in ABG was Corporate Human Resources Manager, where her main responsibilities included Talent Management and Learning & Development and advising ABG's mine sites on Human Resources related processes.
Janet joined ABG as the Human Resources Manager for the Dar es Salaam office and working with specific projects with the mine sites in October 2008. She has worked in different capacities within the Human Resources Function in the company.
Prior to joining ABG, she was the Human Resources Manager for AngloGold Ashanti's Geita Gold Mine where she started her mining industry career after spending 5 years in the aviation industry.
Janet has a Masters Degree in Arts from the University of Dar es Salaam and a Post Graduate Diploma in Management from the Graduate School of Business at the University of Cape Town.
She is a member of the Society for Human Resource Management (SHRM) as well as an affiliate member of the Chartered Institute of Personnel and Development (CIPD).
Janet was a Board member of the Association of Tanzanian Employers (ATE) for the past six years and is currently a Board Member of the Tanzanian Wage Board.

Maisha Yanaedelea

8 df176
Bagamoyo hapa.

Magazeti Tena Na Bukoba Jamii


DSC 0006 2c757
DSC 0010 cc727

DSC 0011 7fee3
DSC 0012 e1b81
DSC 0013 46896
DSC 0014 88cc4
DSC 0015 5ebca
DSC 0016 5f617
DSC 0017 f6af4
DSC 0018 81baa
DSC 0019 39b25

DSC 0008 4c17f
DSC 0009 884b1

Tuesday, April 2, 2013

Kamati Kuu Chadema Kukutana Dar
 Wednesday, 03 April 2013
Published in Siasa
                                TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana kwa siku mbili kwenye kikao chake cha kawaida jijini Dar es Salaam, kuanzia tarehe 3-4 Aprili, 2013.

Katika kikao hicho cha siku mbili, Kamati Kuu itajadili pamoja na mambo mengine, yatokanayo na kikao kilichopita, hali ya kisiasa nchini, pia itapokea taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha Baraza Kuu kilichofanyika mwezi Februari mwaka huu, ikiwemo mpango wa uendeshaji chama kwa kanda.

Aidha, Kamati Kuu pia itajadili mpango kazi na bajeti ya Chama kwa mwaka 2013-2014


Imetolewa Aprili 2, 2013, Dar es Salaam na;

Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari CHADEMA

Wednesday, February 27, 2013

RAIS KIKWETE ATEMBELEA JKT

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na uongozi wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jijini Dar es salaam alipotembelea leo February 27, 2013. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange pia walihudhuria.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa juu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) jijini Dar es salaam alipotembelea leo February 27, 2013. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange pia wapo.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea zawadi ya saa toka kwa  Mkuu  wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Raphael Muhuga huku  Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Vuai Shamsi Nahodha, Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange wakishuhudia. Saa hiyo imeandaliwa na makamanda wa JKT kumpongeza Rais Kikwete kwa kurejesha mafunzo ya jeshi la ulinzi kwa mujibu wa sheria kuanzia mwaka huu.

UZINDUZI WA MPANGO GSI

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikata utepe kuashiria uzinduzi  wa Mpango  Mkakati  wa Miaka Mitano  wa Taasisi  ya  GSI Tanzania  kwenye ukumbi wa hoteli ya Blue Pearl  jijini Dar es salaam Februari 27, 2013. Wapili kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dr.Abdallha Kigoda. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Joyce Mapunjo.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama mikoba katika maonyesho yaliyoambatana na Uzinduzi wa  Mpandgo Mkakati wa Miaka  Mitano wa Taasisi  ya GSI Tanzania kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl jijini Dar es slaam Februari  27, 2013. Kushoto ni Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko, Abdallah Kigoda na kulia ni  Katibu  Mkuu wa Wizara hiyo, Joyce Mapunjo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Tuesday, February 26, 2013

MANDHALI YA CHAMA CHA MSINGI MWEYANJALE KINACHOUNDA KCU 1990 LTD

 Jengo la chama cha msingi cha Mweyanjale kinachojihusisha na kilimo cha kahawa hai 'organic coffee' kinachounda chama cha ushirika Kagera (KCU 1990 LTD).
 Mwenyekiti wa chama hicho, Leopord Mtalemwa akiwa nje ya jengo la chama hicho.
 Maeneo yanayozunguka chama hicho.
Mtalemwa akiongea na waandishi wa habari.

Monday, February 25, 2013

NDANI YA MANISPAA YA BUKOBA KWAWAKA MOTO

MANISPAA ya Bukoba hapakaliki, hii inafuatia hatua ya madiwani wa manispaa hiyo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kususia kikao chama hicho ambacho hufanyika kabla ya kikao cha baraza la madiwani.


Baadhi ya madiwani wa CCM wamesusia kikao hicho baada ya watu wasiofahamika kusambaza waraka unaowakashfu.


Waraka huo unawakashfu madiwani kumi ambao ni pamoja na madiwani wa CCM 8 na wa vyama vya vya upinzani vinavyowaunga mkono 2.


Mwandishi wa waraka huo anatoa kashfa nzito kwa madiwani waliosaini waraka wa kutaka Mstahiki Meya wa manispaa ya Bukoba Anatory Amani apigiwe kura za kutokuwa na imani naye kufuatia tuhuma mbalimbali zinazomkabili.


Baadhi ya madiwani waliiongea walidai mgogoro ulioko kati ya Meya huyo na madiwani kuwa umeishaigawa CCM, kwa anyakati tofauti walisema kuwa hawana imani na meya huyo na ndio maana wanataka kumng'oa.


Walisema kuwa hata kama nyaraka zikisambazwa na kuwakasfu kamwe hawatarudi nyuma, "tunajua waraka huu aliyeuandaa hivyo hatuna wasiwasi nao, moto wetu uko palepale wa kumuondoa Amani madarakani" walisema bila kutaka majina yao yatakjwe.

Walisema kuwa hawataki kuongozwa na kiongozi yoyote mwenye huruka ya ufisadi ambaye anabuni miradi mingi kwa maslahi yake binafsi," Kiongozi yoyote atakayekuwa na mlengo wa kutaka kuifilisi manispaa tutakula naye sahani moja" walimaliza.


Manispaa ya Bukoba sasa kumewaka moto, pande zote zinazopingana kila mmoja anijiona ni mbabe, pande zinazopingana moja unaundwa na kundi la waziri wa maliasili na utalii, Balozi Khamis Kagasheki na upande nyingine inaongozwa ana Meya wa manispaa ya Bukoba Anatory Amani.

Kambi ya Kagasheki inamtaka Meya wa manispaa ya Bukoba Amani anga'atuke na kambi ya Amani inapinga mapendekezo hayo.



WAZIRI PINDA AKUTANA NA BALOZI WA CANADA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akisalimiana na Balozi wa Canada nchini, Mhe.Alexandre Leveque kabla ya mazungumzo yao, Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Februari 25, 2013. (Picha na Ofisi a Waziri Mkuu)

VIONGOZI WASAINI MPANGO WA AMANI WA UMOJA WA MATAIFA

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maal: umu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini  Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 24, 2013
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe Ban Ki-moon akiweka saini Mpango wa Umoja wa Mataifa wa Amani, Usalama na Ushirikiano katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati wa hafla hiyo maal: umu iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika mjini  Addis Ababa, Ethiopia, leo Februari 24, 2013

Monday, February 18, 2013

WAJERUMANI WATOA MSAADA WA VITABU VINAVYOELEZEA HISTORIA YA TANZANIA

 Mfano wa nyumba ya msonge iliyokutwa kwenye jengo la mambo ya kale inayomilikiwa na kampuni ya utalii ya Kiroyera.
 Meneja uendeshaji wa kampuni ya utalii ya Kiroyera, William Rutta akiangalia vitabu vilivyotolewa na Mrs.Edith Gottschling raia wa Ujerumani ambaye mme wake marehemu Klaus alikuwa mwenyekiti wa kwanza wa urafiki kati ya nchi ya Ujerumani na Tanzania.
 Yusto Mchuruza aliyekabidhi vitabu vilivyotolewa nba mjerumani akitoa ufafanuzi wa vitabu hivyo.
 Mambo ndania ya jumba linalohifadhi mambo ya kale.
 Yusto Mchuruza akimkabidhi vitabu William Rutta.

Saturday, February 16, 2013

SOMO LA DINI NA MAADILI KUFUNDISHWA RASMI SHULENI NA VYUONI TANZANIA NZIMA



MIKOA ya Kagera na Kigoma imezindua rasmi mihtasari  ya  somo la Dini na Maadili litakalofundishwa kuanzia shule za awali, msingi sekondari hadi vyuo vikuu.

Mihtasari hiyo imezinduliwa  rasmi na UMAKA (Umoja wa Madhehebu Kagera) wakishirikiana na serikali baada ya mihtasari hiyo kupitishwa rasmi na Kamishina wa Elimu ili isambazwe katika shule zote tayari kwa kutumika kufundishia wanafunzi katika ngazi mbalimbali.

Somo la Dini na Maadili limerasimishwa rasmi kufundishwa shuleni na vyuoni baada ya UMAKA kuona umuhimu wa kuwa na mihtasari ambayo ni rasmi na inayotambuliwa na serikali kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ili itumike kufundishia watoto pia na kutahiniwa kama masomo mengine.

Umoja wa Madhehebu Kagera  (UMAKA) ulianzisha mchakato wa kuandaa mihtasari ya somo la Dini na  Maadili  wakishirikiana na serikali ili somo hilo liwe na mihtasari inayofanana katika kufundishia wanafunzi kuliko hapo awali ambapo somo hilo halikuwa na mihtasari ya kufundishia.

Kupitia somo la Dini na Maadili, wanafunzi  watafunzwa maadili mema ya kupendana na kuwapenda watanzania wenzao, kujenga jamii yenye kuwajibika na kumcha Mwenyezi Mungu bila kujali tofauti za ki-imani kwao, pia kulelewa na kukua katika malezi ya kufuata sheria na utawala bora.

Serikali katika kuboresha utumiaji wa Mihtasri mipya ya somo la Dini na Maadili imeagiza somo hilo likaguliwe na wakaguzi wa serikali pamoja na walimu wakuu wa shule kama masomo mengine na kutahiniwa katika ngazi zote hadi ile ya taifa.

Pia katika kuona umuhimu wa somo la Dini na Maadili kufundishwa shuleni, serikali imeamua mihtasari ya somo hilo itumike Tanzania nzima badala ya Mikoa ya Kagera na Kigoma walioshirikiana na serikali kuandaa mihtasari hiyo  ili wanafunzi wote wa Tanzania wafunzwe dini na maadili ya kitanzania.

UMAKA ilianzishwa miaka ya 1980 ikiwa na lengo la kushirikiana na Serikali na kushauri masuala mbalimbali yahusuyo maadili, amani, usalama na maendeleo ya jamii ya watanzania. UMAKA inajumuisha  Balaza la Maaskofu Tanzania (TEC),  Balaza la Waislam Tanzania (BAKWATA), na Baraza la Wakristo Tanzania (CCT).

MKUTANO WA UZUNDUZI WA SOMO LA DINI NA MAADILI KAGERA

 Baba Askofu Nestory Timanywa Jimbo Katoliki La Bukoba  Ambaye Amestaafu hivi Karibuni Akitoa Mada ya Historia ya Maadili Tanzania Ambapo Alisistiza sana Uwajibikaji wa Wazazi, Walezi na Viongozi Mbalimbali Kuwajibika Kuwalea Watoto katika Maadili Mazuri.
 Wajumbe wa Kikao cha Uzinduzi wa Mihtasari ya  Somo la Dini na Maadili Wakisiliza kwa Makini na Utulivu.
Hawa ni Viongozi wa Dini Mkoani Kagera Waliohudhuria Uzinduzi Mihtasari ya Somo la Dini na Maadili,Katikati Kutoka Kulia Ni Askofu Elisa Buberwa KKKT, Askofu Nestory Timanywa Jimbo Katoliki la Bukoba, Askofu Severine Niwemugizi Jimbo Katoliki la Rulenge, Nyuma Kabisa ni Masista na Mapadre Kutoka Kigoma, na Mstari wa Kwanza ni Viongozi wa BAKWATA Mkao wa Kagera.

mama kikwete aendelea na ziara lindi

IMG_8445
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwasalimia watoto na wananchi wa kata ya Msinjahili waliohudhuria mkutano wa hadhara kwenye kijiji cha Kitumbikwela kilichoko katika wilaya ya Lindi Mjini tarehe 17.2.2013


IMG_8485Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wa Kata ya Msinjahili wakishangilia wakati wa mkutano wa hadhara ulihutubiwa na Mjumbe wa NEC wa wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete katika kijiji cha Kitumbikwela tarehe 17.2.2013.
IMG_8499Wanachama wapya wa Chama Cha Mapinduzi na jumuia zake wakila kiapo mara baada ya kukabidhiwa kadi na Mjumbe wa NEC wa Lindi Mjini Mama Salma Kikwete katika kijiji cha Kitumbikwela tarehe 17.2.2013.
IMG_8525
Mjumbe wa NEC wa Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wananchi wa kata ya  Msinjahili kwenye kijiji cha Kitumbikwela tarehe 17.2,2013.
 PICHA NA JOHN LUKUWI