Wednesday, May 16, 2012

Jk Akimpa Nape Maelekezo

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akimwagiza jambo, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye wakati wa semina ya kuwajengea uelewa wa Utawala bora, Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, iliyofanyika jana May 15, 2012, kwenye ukumbi wa Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Semina hiyo iliandaliwa na Mpango wa Hiari wa Nchi za Umoja wa Afrika kujipima kwa vigezo vya Utawala Bora-APRM. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama. (Picha na Bashir Nkoromo)



News




Saturday, May 12, 2012

Chuo Cha Mafunzo Ya Udereva Lake Zone Driving School Chanufaisha Wakazi Wa Mkoa Wa Kagera

 Kaimu Kamanda Wa polisi mkoani Kagera Vitus Mlolere akifunga mafunza ya awali ya waendesha Pikipiki na Magari katika kata ya Kyebitembe na Karambi ambayo yalieneshwa na Chuo cha Lake Zone Driving School cha Mkoani Kagera.
 Hapa anafunga mafunzo mengine katika kata ya Nshamba iliyoko wilayani Muleba Mkoani Kagera ambapo jumla ya wahitimu arobaini walipatiwa mafunzo hayo kutoka Lake zone
 Mkurugenzi wa Chuo Cha Lake Zone Driving School Winstoni Kabantega akitoa ufafanuzi juu ya mafunzo waliyoyapata wahitimu wa kata za Kyebitembe na Karambi
Kabantega akitoa ufafanuzi tena katika kufunga mafunzo ya kata Nshamba wilayani Muleba
 Wahitimu wa mafunzo ya awali ya udereva wa kata ya Kyebitembe na Karambi wakisoma risara kwa mgeni rasimi hayupo pichani mafunzo hayo yalitolewa na Chuo cha udereva cha Lake Zone Driving School
 Wahitimu wa mafuzo ya awali ya udereva kutoka kata ya Nshamba wakisoma risara
Moja wa askari wa Kikosi cha usalama barabarani mkoani Kagera PC Joseph akiwaapisha wahitimu wa mafunzo ya awali ya udereva yaliyofungwa katika wilaya ya Muleba Mkoani Kagera

Wednesday, May 9, 2012

Wakuu Wa Wilaya Watangazwa

Uteuzi wa Wakuu wa Wilaya Wapya

MAJINA YA WAKUU WA WILAYA WAPYA 70 NA
NA.
 
KITUO CHA KAZI
1.Novatus MakungaHai
2.Mboni M. MgazaMkinga
3.Hanifa M. SelunguSikonge
4.Christine S. MndemeHanang
5.Shaibu I. NdemangaMwanga
6.Chrispin T. MeelaRungwe
7.Dr. Nasoro Ali HamidiLindi
8.Farida S. MgomiMasasi
9.Jeremba D. MunasaArumeru
10.Majid Hemed MwangaLushoto
11Mrisho GamboKorogwe
12.Elias C. J. TarimoKilosa
13.Alfred E. MsovellaKiteto
14.Dkt. Leticia M. WariobaIringa
15.Dkt. Michael Yunia KadegheMbozi
16.Mrs. Karen Yunus Sengerema
17.Hassan E. MasalaKilombero
18.Bituni A. MsangiNzega
19.Ephraem Mfingi MmbagaLiwale
20.Antony J. MtakaMvomero
21.Herman Clement KapufiSame
22.Magareth Esther MalengaKyela
23.Chande Bakari NalichoTunduru
24.Fatuma H. ToufiqManyoni
25.Seleman LiwowaKilindi
26.Josephine R. MatiroMakete
27.Gerald J. Guninita Kilolo
28.Senyi S. NgagaMbinga
29.Mary TeshaUkerewe
30.Rodrick MpogoloChato
31.Christopher MagalaNewala
32.Paza T. MwamlimaMpanda
33.Richard MbehoBiharamulo
34.Jacqueline LianaMagu
35.Joshua MirumbeBunda
36.Constantine J. KanyasuNgara
37.Yahya E. NawandaIramba
38.Ulega H. AbadallahKilwa
39.Paul MzindakayaBusega (mpya)
40.Festo KiswagaNanyumbu
41.Wilman Kapenjama NdileMtwara
42.Joseph Joseph MkirikitiSongea
43.Ponsiano NyamiTandahimba
44.Elibariki Immanuel KinguKisarawe
45.Suleiman O. KumchayaTabora
46.Dkt. Charles O. F. MlingwaSiha
47.Manju MsambyaIkungi (mpya)
48.Omar S. Kwaangw’Kondoa
49.Venance M. MwamotoKibondo
50.Benson MpesyaKahama
51.Daudi Felix NtibendaKaratu
52.Ramadhani A. ManenoKigoma
53.Sauda S. MtondooRufiji
54.Gulamhusein KifuMbarali
55.Esterina KilasiWanging’ombe (mpya)
56.Subira MgaluMuheza
57.Martha UmbulaKongwa
58.Rosemary KiriginiMeatu
59.Agness HokororoRuangwa
60.Regina Chonjo Nachingwea
61.Ahmed R. KipoziBagamoyo
62.Wilson Elisha NkhambakuKishapu
63.Amani K. MwenegohaBukombe
64.Hafsa M. MtasiwaPangani
65.Rosemary Staki SenyamuleIleje
66.Selemani Mzee SelemaniKwimba
67.Lt. Col. Ngemela E. LubingaMlele (mpya)
68.Iddi KimantaNkasi
69.Muhingo Rweyemamu Handeni
70.Lucy MayengaUyui


MAJINA 63 WAKUU WA WILAYA WA ZAMANI NA
VITUO VYAO VYA KAZI
NA.JINAKITUO CHA KAZI
1.James K. O. MillyaLongido
2.Mathew S. SedoyekaSumbawanga
3.Fatuma L. KimarioIgunga
4.Capt. (Mst.) James C. YamunguSerengeti
5.Lt. (Mst.) Abdallah A. KihatoMaswa
6.Sarah DumbaNjombe
7.Jowika W. KasungaMonduli
8.Elizabeth C. MkwasaBahi
9.Col. Issa E. NjikuMisenyi
10.John B. HenjeweleTarime
11.Elias W. LaliNgorongoro
12.Raymond H. MushiIlala
13.Francis MitiUlanga
14.Evarista N. KalaluMufindi
15.Mariam S. LugailaMisungwi
16.Anna J. MagowaUrambo
17.Anatory K. ChoyaMbulu
18.Fatma Salum AllyChamwino
19.Deodatus L. KinawiroChunya
20.Ibrahim W. MarwaNyang’hwale (mpya)
21.Dkt. Norman A. SigallaMbeya
22.Moshi M. Chang’aMkalama (mpya)
23.Jordan M. RugimbanaKinondoni
24.Georgina E. BundalaItilima (mpya)
25.Halima M. KihembaKibaha
26.Manzie O. MangochieGeita
27.Abdula S. LutaviNamtumbo
28.Zipporah L. PanganiBukoba
29.Dkt. Ibrahim H. MsengiMoshi
30.Col. Cosmas KayomboKakonko (mpya)
31.Lembris M. KipuyoMuleba
32.Elinasi A. PallangyoRombo
33.Queen M. MloziSingida
34.Juma S. MadahaLudewa
35.Angelina MabulaButiama (mpya)
36.Hadija H. NyemboUvinza (mpya)
37.Ernest N. KahindiNyasa (mpya)
38.Peter T. KiroyaSimanjiro
39.John V. K. MongellaArusha
40.Baraka M. KonisagaNyamagana
41.Husna MwilimaMbogwe (mpya)
42.Sophia E. MjemaTemeke
43.Francis IsaacChemba (mpya)
44.Abihudi M. SaideyaMomba (mpya)
45.Khalid J. MandiaBabati
46.Anna Rose NyamubiShinyanga
47.Dani B. MakangaKasulu
48.Amina J. MasenzaIlemela
49.Mercy E. SillaMkuranga
50.Christopher R. KangoyeMpwapwa
51.Lt. Edward O. LengaKalambo (mpya)
52.Halima O. DendegoTanga
53.Lephy B. GembeDodoma
54.Saidi A. AmanziMorogoro
55.Jackson W. MsomeMusoma
56.Elias C. B. GoroiRorya
57.Lt. Col. Benedict KitengaKyerwa (mpya)
58.Erasto SimaBariadi
59.Nurdin H. BabuMafia
60.Khanifa M. KaramagiGairo (mpya)
61.Gishuli M. CharlesBuhigwe (mpya)
62.Saveli M. MakettaKaliua (mpya)
63.Darry RwegasiraKaragwe




OFISI YA WAZIRI MKUU,
DAR ES SALAAM.

9 MEI 2012

VITUO VYAO VYA KAZI

Uvccm Kagera Inapokosa Imani Na watendaji Wake

Kagera 
 KAMATI ya utekelezaji ya Jumuiya ya Umoja wa vijana wa Chama Cha Mapindizi (CCM) MKoa wa Kagera (UVCCM) imemkataa katibu wa UVCCM wa Wilaya ya Karagwe kutokana na tuhuma za kushindwa kuwajibika kikamilifu katika shughuli za chama.
 
 
Kauli hiyo ilitolewa jana na mwenyekiti wa UVCCM Mkoa huo Deusidedith Katwale wakati akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za CCM mkoani humo.
 
Katwale alisema katika kikao cha kamati ya utekelezaji ya UVCCM mkoa kimeridhia kumkataa Lufunjo Nkinda ambaye ni katibu wa UVCCM Wilaya ya Karagwe kutokana na kushindwa kwake kuwajibika na kukiuka maadili ya Chama chao.
 
Alizitaja baadhi ya tuhuma zinazomkabili katibu huyo kuwa ni pamona na ulevi wa kupindukia,uharibifu wa mali za umma,kuomba michango bila mpangilio na kushindwa kuwaheshimu viongozi na mamlaka zilizo juu yake kichama ambapo pia aliongeza kuwa amekuwa akijipa vyeo ambavyo havipo katika chama cha CCM.
 
“Ukweli anamatatizo makubwa kichama, anajiita katibu wa CCM wa Wilaya idara ya Vijana nafasi ambayo haipo kwenye chama wengine anawambia kuwa yeye ni usalama wa Taifa wa CCM jambo ambalo linatutia doa kama chama ”Alisema Katwale.
 
Alisema kuwa kwa mujibu wa taratibu za Chama na Uvccm katibu huyo ameisha kanywa mara tatu na kushindwa kujirekebisha ambapo mara ya nne aliandikiwa barua na Katibu wa Wilaya kwa ajili ya kumkanya na matokeo yake alimjibu katibu huyo wa Wilaya Anatory Nshange kwa barua ya matusi akimtukana jambo ambalo ni kinyume na taratibu za chama na katiba yake.
 
Alisema kuwa Kamati hiyo ya UVCCM mkoa inawaomba Uvccm makao makuu watumie taratibu za uajiri wamchukue mtu wao na kumpeleka wanakotaka.
 
Kwa upande wake katibu huyo anayetuhumiwa Lufunjo alipohojiwa na waandishi wa habari juu ya tuhuma hizo zinazomkabili alisema kuwa hakuna barua yoyote ambayo aliwahi kutumiwa inayomtuhumu juu ya jambo la aina yoyote na kwamba hajawahi kuitwa kwenye kikao chochote kwa mijubu wa taratibu za jumuiya.
 
“Tuhuma hizo si za kweli mimi nimefanya kazi za kiutendaji katika kata zote arobaini za Wilaya ya Karagwe,kukataliwa na kuondolewa kwangu ni majungu ya baadhi ya wanachama wasiokitakia chama mema.
 
Wakati huo huo kamati hiyo imempongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete kwa usikivu wake na kuteua baraza jipya la mawaziri ambalo wamedai kuwa wanaimani nalo na wameridhika nalo hususani alivyozingatia kuwaingiza vijana katika baraza hilo .
 
mwisho 

Manispaa Ya Bukoba Wathamini Walipa Kodi wenu



Barabra hii iko mtaa wa Kashenye kata ya Kashai Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera imekatika na hivyo kusababisha usumbufu kwa watumiaji barabara hiyo, mtaa wa Kashenye ni moja ya mitaa iliyoko katika manispaa ya Bukoba ambayo imesahaulika mtaa huu ni moja ya mitaa yenye miundo mbinu hatarishi. 


Tuesday, May 8, 2012

Wenye Hati chafu Wawajibishwe Naibu Waziri Wa Maji

Naibu Waziri wa Maji, Bilithin Mahenge akifungua  mkutano wa  mkuu wa  13 wa mwaka wa mamlaka hizo unaendelea kwenye hoteli ya Blue Pearl, Ubungo Plaza
 
 
NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
 
 NAIBU Waziri wa Maji, Binilith Mahenge ameziagiza  bodi za Mamlaka ya Maji safi na  Majitaka mijini   kuwachukulia  watumishi wote  hatua  zinazostahili , ambao  wamesababisha mamlaka zilizopata hati zenye mashaka   katika  Taarifa ya  Ukaguzi wa Hesabu za Mamlaka hizo kwa mwaka fedha uliopita(2010/2011).
 Kauli hiyo imetolewa leo(jana) na Naibu Waziri huyo wakati alipofungua mkutano mkuu   wa 13  wa mamlaka hizo unaendelea kwenye hoteli ya Blue Pearl, Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam. Mkutano huo wa siku mbili umehusisha  watu 200 ambao ni  wakurugenzi, watalaamu wa  wizara hiyo, TAMISEMI, Wenyeviti wa Bodi na Watendaji  Wakuu wa  EWURA, DAWASA na DAWASCO  na wadau wengine.
Mada kuu ya mkutano huo ni “Kuzijengea Mamlaka  Uwezo wa Rasilimali watu katika Kutoa Huduma Endelevu”
“ Ukaguzi  wa Hesabu za Mamlaka na ripoti zake ni kioo muhimu cha kupima uttendaji kazi, usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma kwenye mamlaka… Sikuridhika na kiwango cha kuongezeka   mamlaka zilizopata hati zenye mashaka  kutoka tatu  mwaka 2009 /2010 hadi tano mwaka 2010/2011. Tegemeo langu mamlaka zote  zipate hati safi ya ukaguzi wa hesabu.  
 Naibu Waziri Mahenge  alizitaja mamlaka hizo kuwa ni Mtwara, Musoma, Songea, DAWASA na DAWASCO, ambapo alizitaka kuongeza nguvu katika usimamizi wa fedha katika mamlaka zao kwa kuhakikisha hesabu za mamlaka hizo zinatayarishwa kwa usahihi  unaokubalika n kuondoa kasoro zilizojitokeza.
Aidha Mahenge aliongeza kuwa kasi ndogo ya utekelezaji wa program ya miradi ya maji  iliyopangwa inachangiwa na uhaba wa fedha kwa kiasi kikukubwa na upungufu wa wataalamu wanaoweza kusimamia kwa makini utekelezaji wake kuanzia ngazi za mikoa , wialya, miji midogo na miradi ya kitaifa.
Aliyataja maeneo yenye upungufu kuwa ni  usimamizi fedha za miradi, ununuzi, utoaji taarifa za utekelezaji wa miradi, ukusanyaji na utoji wa taarifa za miradi, uchambuaji na utunzaji takwimu.
Alisema hali hiyo inaonyesha umhimu wa kujenga uwezo kwa watendaji katika ngazi zote ili mapungufu yaliyopo yasiendelee kuonekana, hivyo alizitaka bodi hizo kuwa na mipango ya mafunzo inayotekelezeka na kulenga mapungufu hayo.
Mahenge alisema changamoto nyingine  katika utkelezaji wa program ya maendele ya sekta ya maji ni kuchelewa kwa fedha za maendeleo kutoka wadau wa maendeleo, hali ambyo imesababisha  wakandarasi kupunguza kasi ya ujenzi na kutoza riba, ikiwemo kuchelewa kukamilika kwa ujenzi.
Alisema uchelewaji wa malipo unatokana na hasa na uchelewashaji wa taarifa za utekelezaji kutokakwa watekelezaji wa ngazi zote. Hivyo hadi kufikia Aprili mwaka huu jumla ya sh. bilioni 32.7 hajijalipwa kati ya hizo fedha za wakandarasi ni sh. bilioni 30.1 na wahandisi washauri ni sh. bilioni 2.6.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mhadisi Christopher Sayi alisema  katika jiji la Dares Salaam na maeneo yanayohudumiwa na DAWASCO, kiwango cha utaoji wa huduma ya majisafi kimeshuka na kufikia asilimi 51kipindi cha mwezi Juni,2011 kutoka asilimia 55 ya Juni 2010.
Alisema upungufu huo umetokana na kupungua kwa uzalishajimaji uliosababishwa na  mgao wa umeme na ongezeko la maeneo ya utoaji huduma kwa kupanuka kwa jiji.
Na Magreth Kinabo MAELEZO

Taarifa Ya Jana Kutoka CCM

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Hivi karibuni chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kilielezea kile ilichoeleza kuwa ni kutishwa na wimbi la mauaji yanayotishia amani ya nchi kikidai kuwa jumla ya wanachama wake 15 wameuawa katika wilaya ya Igunga peke yake.

Madai hayo ya CHADEMA, pamoja na wanachama wengine na mashabiki wao, yalitolewa na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, ambaye alidai kuwa mauaji hayo yana mkono wa serikali ya CCM, ambayo kwa madai yao imeona wazi kuwa upepo wa kisiasa umekiendea vibaya na sasa kinataka kujiimarisha katika utawala kwa kuua watu wanaoipinga.

Akifungua kikao cha Baraza Kuu la chama hicho jijini Dar es Salaam Aprili 29 mwaku huu mwenyekiti huyo alifafanua kuwa mbali na kuuawa kwa watu wanne kwa pamoja na juzi kifo cha mwenyekiti wao wa tawi huko Arumeru mkoani Arusha, jumla ya wanachama wake 15 wameuawa katika wilaya ya Igunga peke yake tangu kumalizika kwa uchaguzi mdogo wa jimbo hilo mwaka jana.

Mbowe katika maelezo yake alijaribu katika maeneo kadhaa kuihusisha CCM na au serikali yake katika matukio kadhaa yaliyowakabili baadhi ya wanachama na viongozi wa Chadema katika maeneo mbalimbali nchini likiwemo lile la Mbunge Highness Kiwia ambaye Suala lake bado Lipo mikononi mwa vyombo Vya dola likishughulikiwa.

Katika sehemu kubwa ya maelezo ya Ndg. Mbowe amejitahidi kuonesha kuwa mauaji yote yaliyoikabili na yatakayokuwa yakiikabili Chadema kupitia wafuasi wake yanafanyika kisiasa, Jambo ambalo ni la uzushi, kwani Halina ushahidi wa kisheria hata kimazingira, wa Moja kwa Moja unaoondosha ujinai au makosa hayo, na kuwa ni makosa yanayolenga muktadha wa kisiasa.

Huku akitaka kuuaminisha umma kuwa huo ndio ukweli, Ndg. Mbowe amesisitiza kuwa hilo lime kuwa likitekelezwa na CCM kwa lengo la kuwatisha wananchi kujiunga na chama hicho hoja ambayo haina msingi wowote wa kiutafiti.

Hivyo CCM kwa kutambua kuwa Suala la mauaji linabeba Kosa la jinai, na kwa kuwa Ndg. Mbowe ameshutumu Moja kwa Moja CCM na serikali yake kuihusisha na mauaji hayo, ni vema sasa nasi tukatoa msimamo wetu dhidi ya tuhuma, hiyo.

Kwanza, si busara hata kidogo kuihusisha CCM katika matukio hayo, kwani uchunguzi unaofanywa na vyombo vya dola umeshindwa mpaka sasa kuhusisha matukio hayo na siasa, badala ya kuyahusisha na makosa ya jinai ambayo hufanywa na watu kwa malengo tofauti na yale ambayo Ndg. Mbowe anataka kuwaaminisha watu.

Pili, CCM haijawai, haiwezi, na haitakuja fanya jambo lolote lenye lengo la kuvuruga Amani na Usalama wenye utulivu ndani ya taifa letu, hivyo uzushi na usingiziaji uliofanywa na Mtu Kama Ndg. Mbowe, si vema kuuacha kimya, badala yake nimetumia wasaa Huu muhimu Kujibu, na kutoa ufafanuzi ili Kuupa umma wa watanzania habari sahihi.

Ni aibu kwa Chama kama Chadema kujitahidi kwa nguvu zote kujaribu kuficha ukweli wa mauaji yanayotoa roho za watanzania wenzetu kwa kuyapa sura ya kisiasa. Hizi ni juhudi za makusudi za kutaka kuficha ukweli wa kinachotokea.

Ni aibu kwa chama kama Chadema kujaribu kutumia mauaji mabaya kama haya kutafuta mtaji wa kisiasa. Huku ni kuonyesha jinsi gani wamefilisika kisiasa mpaka wanafikia mahali pa kuamini kuwa wanaweza kutumia chochote kama mtaji wa kisiasa, vikiwemo vifo vya watanzania wenzetu. Huku si kufilisika tu ila kwakweli ni unyama unaotakiwa kulaaniwa na kila muungwana.

Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM

News Papers Zinasema Je?




By Mjengwa Blogspot

Waandishi Wa habari Kagera Wafundwa na Mkuu Wa mkoa


 
Bukoba
 
Kanal mstaafu Fabiani Massawe ni mkuu wa mkoa wa kagera  amewashauri wanachama na waandishi wote mkoani humu kuandika habari za uchunguzi wakifuata misingi,maadili na kanuni za uandishi wa habari ili kufanya kazi yao kuwa nyepesi na isiyokuwa na migongano isiyokuwa ya lazima.
 
Massawe aliwashauri waandishi kuandika habari za uhakika kwa kutumia vyanzo sahihi kabla ya kuandika habari na kutoandika habari zinazopendelea upande mmoja na zenye maslahi binafsi ili kuepuka kusababisha migawanyiko ndani ya jamii inayoweza kusababisha uvunjifu wa amani   ambapo alitoa mfano wa vita vya Kimbali vilivyosababishwa na uchochezi wa baadhi ya vyombo vya habari huko nchini Rwanda.
 
Aliwataka waandishi kuacha tabia ya kuomba mishiko au bahasha ndipo waandike habari kwa madai kuwa tabia hiyo ni kujidhalilisha na kuonekana waandishi ni watu wa kulalamika kila wakati kuwa hawana kitu jambo ambalo ameziomba klabu na waajiri wa vyombo mbalimbali kulifanyia kazi kwani ni kero inayowafanya watoa habari kujenga uadui na waandishi kwa madai kuwa wamekuwa wakitishia kuwa wakinyimwa mishiko hawaandiki habari ya aina yoyote.
 
Pia amewashauri waajiri wa vyombo mbalimbali vya habari hususani radio za kijamii zipatazo tano za mkoa wa Kagera kutafuta utaratibu wa kuwaondoa waandishi makanjanja ambao wamekuwa wakiajiriwa kwani wanalipwa ujira mdogo huku waandishi wenye ujuzi na kazi hizo wakikosa nafasi jambo ambalo amedai kuwa matokeo yake wamekuwa wakitumia radio hizo kujadili maisha ya watu na kuongea mambao yasiyofaa katika jamii huku wengine wakitangaza habari za mapenzi tu wakati kuna habari zinazogusa jamii mfano wahamiaji haramu na rushwa hazipati nafasi jambo ambalo amedai kuwa ni kuidhalilisha taaluma hiyo muhimu.
 
Kanal Massawe alikuwa mgeni rasmi katika sherehe za kuadhimisha sikuukuu hiyo ya uhuru wa vyombo vya habari ambapo kwa mkoa wa Kagera ilifanyika katika ukumbi wa Coffee Tree in ndani ya Manispaa ya Bukoba na kudhaminiwa na muungano  wa vilabu vya waandishin wa habari nchi (UTPC)na kuudhuliwa na viongozi mbalimbali wa mkoa huo ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti wa bodi ya kahawa nchini Pius Ngeze,Kamanda wa Takukuru mkoa Domina Mkama,Kaimu kamanda wa polisi mkoa Vitus Mlorele,mkuu wa Wilaya ya Bukoba Samweli Kamote na viongozi wa vyama vya siasa mkoa na Wilaya.
 
Aidha  mkuu huyo wa mkoa aliiahidi kuwachangia kiasi cha shilingi milioni moja kama mchango wa kununulia kiwanja cha kujenga ofisi ya klabu hiyo ili waweze kuondokana na  usumbufu wanaoupata wa kupanga kwenye majumba ya watu ambapoa wamekuwa wakiwasumbua mara kwa mara pasipokuwa na sababu za msing .
 
Katika hatua nyingine klabu ya Waandishi wa habari mkoani Kagera (KPC) imetoa msaada mbalimbali katika wodi za wagonjwa katika hospitalia ya mkoa wa Kagera.
 
Tukio hilo lililifanyika May 5 katika hospitali hiyo kwa kukabidhi misaada mbalimbali katika wodi za watoto hospitalini hapo.
 
Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoani Kagera John Rwekanika alisema kuwa wanachama wa KPC wapatao 34 wamelazimika kutoa misaada hiyo katika tamasha lao lakuadhimisha uhuru wa vyombo vya habari duniani iliyoadhimishwa mei 5 badala ya mei 3 mwaka huu inayoadhimishwa kila mwaka kutokana na wanachama na wanachama wengi kukabiliwa na majukumu mwengi katika tarehe rasmi inayoadhimishwa ulimwenguni.
 
Alisema kuwa misaada iliyotolewa ni pamoja na sabuni,sukari na biskuiti vyote vyenye thamani ya shilingi laki 2 ambapo vyote viligawiwa katika wodi za watoto ambazo alizitaja kuwa ni namba saba yenye wodi mbi A na B tofauti na kuwa jumla ya watoto 55 waliolazwa katika hospitalia hiyo wamepokea misaada.
 
Alisema kuwa waandishi wa habari ni sawa na taasisi au jumuiya yoyote ya kirai inyopaswa kushirikiana na raia katika shughuli zote za kijamii kuwa kutokana na chama chao kuwa na ushirikiano wa dhati wameonelea kutumia fursa hiyo kuungana na wagonjwa,wazazi na wauguzi wa hospitali hiyo.
 
Kwa upande wake kaimu mganga mfawidhi wa hospitalia hiyo Dk.Leonce Mboyerwa alisema kuwa kitendo kilichofanya na waandishi wahabari hao wa Klabu hiyo ni cha kizalendo na kuwa kimeonyesha ni kiasi gani waandishi walivyo na mchango mkubwa katika jamii.
 
Mboyerwa aliongeza kuwa waandishi wa habari wanafanya kazi katika mazingira magumu lakini wameweza kuonyesha moyo wao wa upendo katika maadhimisho yao ya uhuru wa vyombo vya habari kwa kuungana na jamii inayowategemea kuwa hata taasisi nyingine za Kiserikali na zisizo za Kiserikali wanapswa kuiga mfano uliotolewa na wanachama na uongozi wa KPC.
 
Aidha mmoja wa wazazi katika Wodi ya watoto namba saba A Joyce Rweyemamu alisema waandishi wa habari wameonyesha kitendo cha utu na kuwa wameionyesha jamii kuwa wao ni kioo cha jamii.
 
Alisema kuwa pamoja na misaada walioipokea kutoka kwaandishi hao kuwa wawapo katika hospitali hiyo wanakabiliwa na changamoto ya kukosekana kwa madawa na kuwa mgonjwa aliyelazwa analazimika kujinunulia madawa ambapo wagonjwa wengine wanakuwa hawa uwezo wa kujinunulia madawa kuwa jambo hilo linadhiri afya na kusababisha vifo vya mara kwa wagonjwa.
 
Naye mku wa idara ya watoto hospitalia ya mkoa wa Kagera Gerad Kabyemera alikiri kuwepo kwa hari hiyo ya upungufu wa madawa na kuwa tatizo hilo halisababishwi na uongozi wa hospitali balia linasababishwa na stoo kuu ya madawa makao mkauu ya afya Dar Es Salaam.
 
Kabyemera alisema kuwa uongozi wa hospitali unaomba wastani wa asilimia 100 ya madawa kutoka makao makuu lakini wanatumiwa wastani wa asilimia 40 ya madawa walioomba ambayo hayawezi kutosheleza mahitaji ya wagonjwa kulingana na idadi ya wagonjwa wanaolazwa katika hospitali hiyo.
 
 mwisho

Monday, May 7, 2012

Mkapa Amuunguza Rais Kikwete

•  Waliotemwa uwaziri wamsusa

na Mwandishi wetu


RAIS mstaafu, Benjamin Mkapa, jana aliikaanga serikali ya Jakaya Kikwete mahakamani akidai kuwa hakuna ubadhirifu wowote uliofanywa na aliyekuwa Balozi wa Italia, Prof. Costa Mahalu, katika ununuzi wa jengo la ubalozi nchini humo.
Akiongozwa na wakili wa utetezi, Alex Mgongolwa, baada ya kuapa alieleza kuwa kati ya mwaka 1995-2005 akiwa Rais alifahamu ununuzi wa jengo la ubalozi nchini Italia kwa euro 3,098,741.40, na kuwa hata aliyekuwa Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye ni Rais wa sasa, Jakaya Kikwete alikubaliana na ununuzi huo.
Mkapa ambaye ni shahidi wa Mahalu katika kesi hiyo alisema mwaka 2003 yeye ndiye aliyekwenda mjini Rome-Italia kulizindua jengo hilo la kisasa, Profesa Mahalu akiwa balozi.
“Serikali yangu iliarifiwa bei na taratibu za kulinunua na mimi kama Rais wa nchi nilitaarifiwa kuwa muuzaji alitaka malipo yafanywe mara mbili tofauti katika akanti zake …na mimi kwa niaba ya serikali yangu nikatoa idhini linunuliwe kwa mtindo huo nilioutaja hapo juu,” alidai Rais Mkapa.
Mahalu anatuhumiwa kuidhinisha kwa niaba ya serikali ununua wa jengo la ubalozi kwa thamani ya euro milioni 3 kwa njia ya mikataba miwili na kwa akaunti mbili.
Mawakili: Wewe au serikali ya awamu ya tatu iliwahi kupokea malalamiko toka serikali ya Italia kuwa ubalozi wetu nchini humo ulivunja sheria kuhusu mchakato mzima wa ununuzi wa jengo hilo?
Mkapa: Hapana, sijawahi kupokea malalamiko.
Mawakili: Ukiwa Rais hujawahi kupokea malalamiko kuwa fedha za serikali yetu zilizotumwa kwa ajili ya kumlipa muuzaji wa jengo hilo kuwa hazijamfikia?
Mkapa: Hadi leo hii natoa ushahidi hapa mahakamani sijawahi kupokea malalamiko ya aina hiyo.
Mawakili: Uliwahi kupata malalamiko toka kwa CAG, Wizara ya Mambo ya Nje, Katibu Mkuu Kiongozi, Waziri wa Mambo ya Nje, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wala Ofisi ya DPP kuhusu ubadhirifu wa ununuzi wa jengo hilo?
Mkapa: Sijawahi kupata.
Mawakili: Nini ufahamu wako kuhusu utumishi wa Profesa Mahalu?
Mkapa: Namfahamu kama msomi mzuri, mchapakazi, muadilifu na kiongozi anayetenda haki.
Mawakili: Mawasiliano kati ya serikali na balozi yanafanyika kwa njia zipi?
Mkapa: Balozi anaweza kuwasiliana na serikali yake kwa njia ya barua kwa Wizara ya Mambo ya Nje, Katibu Mkuu Kiongozi, Rais au kwa njia ya mdomo. Na mawasiliano siyo lazima yafanyike kwa njia ya maandishi tu kwa sababu maelekezo mengine ambayo anapewa balozi na serikali yake ni ya siri kwa maslahi ya taifa hivyo anaweza kuitwa nyumbani na kupatiwa maagizo hayo kwa njia ya mdomo.
Mawakili: Kwa wadhifa wako ule wa urais, kabla ya kwenda kuzindua jengo hilo Januari 23, 2003, hukuwahi kupokea taarifa toka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na DPP za kukukataza usiende kuzindua jengo hilo kwa sababu kulikuwa na harufu za ubadhirifu wa fedha za umma?
Mkapa: Ofisi hizo hazikuwahi kunipatia taarifa hizo.
Yafuatayo ni mahojiano baina ya mawakili wa serikali
Mawakili: Hebu ieleze mahakama ni kwa nini bei za jengo zinatofautiana maana risiti za manunuzi zinaonyesha lilinuliwa kwa euro milioni 3 na hansard ya Bunge iliyosomwa na Kikwete bungeni mwaka 2004 inasema ilinuliwa kwa shilingi bilioni 2.9?
Mkapa: Kazi yangu siyo kufanya uthamini wa fedha za kigeni kwamba wakati huo hizo euro milioni 3 zilikuwa na thamani gani kwa fedha Tanzania (kicheka).
Mawakili: Nani aliagiza upelelezi wa manunuzi ya jengo la Italia ufanyike?
Mkapa: Sijui.
Mawakili: Uchunguzi wa jengo hilo ulifanyika wakati wewe ukiwa madarakani?
Mkapa: Sijui, nilikuja kuona Balozi Mahalu kashtakiwa mwaka 2007 nikiwa tayari nimestaafu. Nilithibitisha taarifa hizo kupitia vyombo vya habari kuwa ameshtakiwa.
Mawakili: Nani alikupa taarifa za muuzaji wa jengo hilo anataka kulipwa kwa mtindo huo wa akaunti mbili?
Mkapa: Ni Mahalu na alinipa taarifa kwa mdomo na alikuwa ameandaa ripoti juu ya ununuzi na akawa anaomba ridhaa ya serikali kabla ya kulinunua.
Mawakili: Ulisema hukuweza kuzuia ununuzi wa jengo, je ulikuwa na madaraka ya kuweza kuzuia lisinunuliwe?
Mkapa: Eh! Mimi ndiye nilikuwa Rais wa nchi; nilikuwa na madaraka hayo na badala yake fedha hizo zingeelekezwa kwenye mahitaji mengine ila kwa sababu nilikuwa ninajua umuhimu na faida ya nchi kununua jengo lile ndiyo maana nikaridhia kwa mdomo linunuliwe.
Wakili: Ulitoa maelekezo kwa nani?
Mkapa: Nilitoa maelekezo kwa njia ya mdomo kwa watendaji na maagizo hayo yalipaswa yatekelezwe na Wizara ya Mambo ya Nje na ilikuwa jukumu la Mahalu kuieleza wizara hiyo na ubalozi utekeleze maagizo yangu.
Wakili: Kwa hiyo unaieleza mahakama kuwa Wizara ya Mambo ya Nje, ilituma malipo kwa mtindo wa akaunti mbili tofauti?
Mkapa: Inahusu nini sasa? Mimi nilitoa maagizo, hivyo lilikuwa ni jukumu la Balozi Mahalu kuieleza wizara yake. Sasa suala la hayo makaratasi ya kufanya mchakato wa kulinunua, mimi kama Rais siwezi kuingilia. Watendaji walipaswa watekeleze.
Mawakili: Utajisikiaje tukikwambia kuwa yule muuzaji aliyetuuzia jengo kwa mtindo wa akaunti mbili alikuwa akikwepa kodi kwa serikali ya Italia?
Mkapa: Aaah! Mi’ sioni tatizo; kikubwa hapa Tanzania tumepata jengo, Alhamdulilah (kicheko).
Mawakili: Utajisikiaje ukisikia Mahalu alitumia zile euro milioni 3 kwa matumizi yake binafsi?
Mkapa: Nitashangaa sana. Pia wewe wakili wa serikali ndiyo nitakushangaa zaidi kwani hansard ya Bunge iliyosomwa na Kikwete bungeni imetamka bayana kuwa serikali ilimlipa muuzaji wa jengo na kwamba taratibu na sheria ya manunuzi ya umma zilifuatwa na hadi sasa huyo muuzaji hajawahi kulalamika kuwa hajalipwa fedha zake.
Rais Mkapa aliingia mahakamani hapo saa 3:45 asubuhi akiwa katika gari aina VX lenye namba T 745 BQE akiongozwa na walinzi wake.
Maafisa toka Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) walionekana kuingia katika viwanja vya mahakama hiyo kabla ya kiongozi huyo kuwasili.
Hakimu Mkuu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Ilvin Mugeta, aliahirisha kesi hiyo hadi leo ambapo mshtakiwa wa pili aliyekuwa Meneja Utumishi na Utawala wa Ubalozi huo, Grace ataanza kujitetea
By www.freemedia.co.tz

Rais Jakaya kikwete Awaapisha Mawaziri Jana

  Dk. Harrison Mwakyembe akila kiapo kuwa waziri wa Uchukuzi mbele ya Rais Jakaya Kikwete kwenye viwanja vya Iku asubuhi hii.
 Shamsi Vuai Nahodha akila kiapo kuwa waziri wa Ulinzi mbele ya Rais Jakaya Kikwete.
 Dk Husein Mwinyi akila kiapo kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii mbele ya Rais Jakaya Kikwete
Mh. Mathias Chikawe waziri wa Sheria na Katiba.

Hawa Ghasia akila kiapo

Profesa Jumanne Maghembe akisaini kiapo mara baada ya kuapa kuwa waziri wa  maji na umwagiliaji Picha Na Ikulu

SIKU YA VYOMBO VYA HABARI KAGERA

 Anaitwa Bi Renatha Kipaka akitoa msaada kwa mmoja wa wagonjwa katika Hospitari ya watoto katika Hospitari ya mkoa wa Kagera,Waandishi wa habari walitembelea hospitari hiyo na kutoa misaada mbalimbali.
 Baada ya hapo iliandaliwa pati hapani mkuu wa mkoa wa Kagera kanali msataafu Fabiani Masawe akihutubia wageni waalikwa wakiwemo waandishi wa habari
 Majembe wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Kagera huku wakila mvinyo
Baadhi ya wageni walipata fursa ya kuongea machache juu ya Madia Day